Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ODAMA AJIFUNGUA KIDUME

 
Stori: Imelda Mtema
HABARI njema! Staa wa sinema za Kibongo, Jenifer Kyaka ‘Odama’ amejifungua kidume huku akikataa kumtaja baba wa mtoto huyo.

Staa wa sinema za Kibongo, Jenifer Kyaka ‘Odama’.
anayedaiwa kwamba ni mheshimiwa serikalini.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu makini, Odama alijifungua kwa operesheni hivi karibuni kwenye Hospitali ya Kairuki jijini Dar baada ya kuwa kimya kwa miezi kadhaa kutokana na likizo ya uzazi ambayo ilimfanya asimame kuigiza filamu kwa muda.


Jenifer Kyaka ‘Odama’ akiwa kwenye pozi.
Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, gazeti lilimtafuta kwa njia ya simu ambapo alikiri kujifungua mtoto wa kiume na kwamba anamshukuru Mungu kwani yeye na mwanaye wanaendelea vizuri.
“Namshukuru sana Mungu na mimi sasa naitwa mama. Hayo mengine ya baba mtoto tuyaache muda ukifika mtamuona,” alisema Odama.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top