Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TAARIFA ZAIDI KUHUSU BOMU LILILOLIPUKA NDANI YA GARI


Ripota wa TZA nchini Kenya Julius Kipkoitch anaripoti kwamba ni watu wanne wameuawa baada ya gari lilokua likielekeea katika kituo cha polisi cha Pangani kilometa mbili kutoka Eastleigh jijini Nairobi kulipuliwa na bomu lilokua ndani ya gari hilo.

Mkuu wa polisi kituo cha pangani anasema gari hilo lilisimamishwa na maafisa wa polisi waliolishuku kwa sababu lilikua likiendeshwa kwenye upande wa kulia wa barabara badala ya kushoto.

Maafisa wawili wa polisi waliingia kwenye Gari hilo na kuliongoza hadi kituo cha polisi cha pangani na baadaye bomu lilokua ndani ya gari hilo kulipuka katika eneo la kuegeshea magari katika kituoni humo na kuwaua watu wanne wakiwemo washukiwa wawili.

Walioshudia wanasema magari mawili yaliokua yakifatana kabla ya lile lilokua mbele kulipuka ndani ya kituo cha polisi cha Pangani ambapo bosco Mugendi mmiliki wa kibanda cha kuuza bidhaa eneo la pangani  alinukuliwa na BBC akisema ‘kile kilichonikuta katika kibanda changu ni nyama ya watu iliyonirukia halafu mimi nikatoroka na kutoka nje’ Screen Shot 2014-04-24 at 3.46.49 PMCREDITS: TZA
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top