Ni baada ya kuchelewa kuwasili katika mkutano wao, walihofia kugeukwa baadaye aliwasili na kuwaeleza yaliyojiri. Wajumbe
wa Mkutano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), juzi nusura
wamgeuzie kibao mwenyekiti wao, Freeman Mbowe baada ya kuchelewa kufika
kwenye mkutano ulioandaliwa ikiwa ni siku moja baada ya kususia kikao
cha Bunge la Katiba.Ukawa walikutana kwenye Ukumbi wa African Dream kwa ajili ya kujipanga baada ya kususia mkutano wa Bunge.Mkutano
huo ulioanza saa 4:18 ukiongozwa na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim
Lipumba baadaye wajumbe walianza kuhoji walipo viongozi wao, Freeman
Mbowe na James Mbatia.Mmoja wa
wajumbe wa mkutano huo, Profesa Abdallah Safari alisimama na kuhoji
walipo viongozi hao hatua iliyoanza minong’ono miongoni mwa wajumbe
wakiwa na hisia kwamba huenda wamewageuka na kwenda kwenye Kikao cha
Kamati ya Uongozi.“Tujue kabisa
kama wametugeuka...Tumeshakubaliana hakuna mtu kwenda kwenye Mkutano wa
Kamati ya Uongozi, sasa kama amekwenda tujue,” ilisikika sauti ya mmoja
wa wajumbe.Kuona hivyo,
ilibidi Profesa Lipumba aanze kuwapigia simu huku wajumbe wakiwa kimya
kusikiliza nini kitafuata. Baadaye Profesa Lipumba aliwaambia wajumbe
kuwa ameongea nao wote na wako njiani wanakuja.Baada
kusikiliza taarifa hiyo, wajumbe walianza kutoa hoja mbalimbali. Saa
5:07 waliwasili Mbowe na Mbatia kwa pamoja na kwenda kukaa kwenye nafasi
zao mbele.Mbowe baada ya
kukaribishwa alisema: “Jamani naomba radhi kwa kuchelewa, nilipigiwa
simu na Katibu wa Bunge, John Joel kuwa nahitajika kwenye kikao cha
Kamati ya Bajeti...Nilikwenda kule kwa kuwa nilijua masuala ya bajeti ni
ya kitaifa.“Lakini nilipofika,
nikakutana na Kamati ya Uongozi ya Bunge Maalumu la Katiba, nikawaeleza
kuwa siwezi kukaa kwenye kikao hiki, ingekuwa bajeti kama nilivyoelezwa
sawa lakini hii nawaambia sitashiriki,” alisema Mbowe na kushangiliwa.Baada
ya hapo, Mbowe alieleza msimamo wa Ukawa kuwa hautashiriki Bunge la
Katiba hadi hapo utaratibu utakapobadilishwa wa mwenendo wa Bunge la
Katiba.Hata hivyo, baadaye Mbowe aliwatoa nje waandishi wa habari akisema wawapishe kwa ajili ya kuzungumza mambo yao ya jikoni
.-MWANANCHI
Post a Comment