Kama makombe halisi?, mzigo huu umekamatwa katika mji wa Yiwu tayari kwa safari ya kwenda nchini Libya
Maofisa wa
kuzuia bidhaa zisizo na hati miliki nchini China wamekamata makombe feki
ya kombe la dunia zaidi ya 1,000 katika ghala ya kampuni moja kubwa ya
utengenezaji na usafirishaji wa baidhaa
NDOTO ya mashabiki wa timu ya Taifa ya England `Simba watatu` ni kunyanyua kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
Lakini suala
hili limechukua sura mpya na shukurani za dhati ziwaendee viongozi wa
desturi wa China waliofanikisha kukamata mzigo feki.
Nchi ya China
imekamata makombe feki ya kombe la dunia zaidi ya elfu moja ( 1,000)
katika ghala ya kampuni moja kubwa ya usafirishaji nchini humo.
Makombe hayo
feki 1, 020 ya kombe la dunia yamekamatwa katika mji wa Yiwu, jimbo la
Zhejiang, ambalo ni moja ya miji mikubwa ya usafirishaji wa bidhaa
duniani.
Makombe hayo feki kwa asilimia kubwa yanafanana na makombe halisi ya FIFA na yalikuwa tayari kusafirishwa kwenda nchini Libya.
Mkurugenzi wa
desturi wa China mwenye mamlaka ya kuzuia nyara zisizohalali alianzisha
kampeni mwezi huu wa nne ili kukamata bidhaa zote feki zilizotengenezwa
kuelekea kombe la dunia bila kuwa na hati miliki.
Kombe la dunia
nchini Brazil linatarajia kuwa na biashara kubwa, na China
wameshakamati dili hili na viwanda vyake vimetengeneza bidhaa nyingi za
kombe hilo, lakini kuna wajanja wachache wanaotaka kujinufaisha bila ya
hati miliki.
Nahodha wa
England Steven Gerrard ana matumaini ya kubeba kombe halisi mwaka huu
nchini Brazil ambapo wapo kundi moja na mataifa ya Italia, Costa Rica na
Uruguay.
Credit:ShaffihDaud
Post a Comment