WACHEZAJI
16 kati ya 34 wa kikosi cha Maboresho ya Timu ya Taifa (Taifa stars)
wamechaguliwa kutoka kwenye kambi iliyokuwa ikifanyika katika Uwanja wa
Chuo cha Ualimu Tukuyu Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya .
Kikosi
hicho kimetangazwa leo jijini Mbeya na Kocha Msaidizi, Salum Mayanga,
aliyekuwa na timu hiyo katika Mkutano na waandishi wa Habari uliofanyika
katika ukumbi wa Hoteli ya Hill View iliyopo mjini humo.
Mayanga aliwataja wachezaji hao kuwa ni Mlinda mlango Benedict Tinoko Mlekwa kutoka Mara.
Walinzi wa kati: Emma Namwondo Simwanda kutoka Temeke na Joram Nason Mgeveja kutoka Iringa.
Walinzi
pembeni : Omari Ally Kindamba kutoka Temeke, Edward Peter Mayunga
kutoka Kaskazini Pemba na Shirazy Abdallah Sozigwa kutoka Ilala,viongo
wa Ulinzi ni Yusufu Suleiman Mlipili na Said Juma Ally kutoka Mjini
Magharibi.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com


Post a Comment