Taarifa kwa umma juu ya kutelekezwa na chama changu (NCCR Mageuzi
Ndugu Watanzania na wale wote wanaojali UTU wa mtu, kwa kweli leo imenibidi niseme tu kutokana na hali yangu inavyozidi kuwa mbaya kutokana na chama changu NCCR-Mageuzi kunitelekeza baada ya kupata ajali nikiwa nasimamia uchaguzi wa mdogo wa marudio wa udiwani huku mimi nikiwa mwandamiz wa chama kitengo cha vijana wa NCCR-Mageuzi mwaka jana 2013 kabla sijawa Mjumbe wa Halmashauri kuu mwaka 2014..
Uchaguzi mdogo wa mwaka jana 2013 wa udiwani kata ya Nyampulukano wilayani Sengerema tulipata ajali jumamosi ya kuamkia uchaguzi tukiwa na viongozi wa jimbo la Sengerema mimi nikiwa mbele tukitoka kukagua vituo vya kupigia kura baada ya kuambiwa vimehamishwa na nikiwa ndio msimamizi mkuu wa uchaguzi huo.
Post a Comment