"Sijawahi kuona mwanamke mzuri na mwenye imani kama mama Komba ( Salome ) jamani, unajua kulea watoto ambao mama zao wapo duniani ni kazi sana," alisema Komba katika kipindi cha mkasi kinachorushwa na East African Television
Mheshimiwa
Komba alisema ana watoto tisa wakiwemo wa ndani ya ndoa na
nje ya ndoa na wote wamelelewa na mke wake Salome na ndio
maana anampenda na kumjali kila siku za maisha yake kwani
anastahili kuitwa mwanamke haswa.....
John
Komba aliyasema hayo siku chache baada ya kuonekana picha
zake mbaya za kimahaba alizopiga akiwa na msichana anayedaiwa
kuwa ni mpenzi wake.....
Katika
mahojiano na kipindi cha Mkasi, John Komba aliongelea mambo
mengi na kusema kuwa ukiwa kiongozi na mtu mkubwa nchini ni
lazima uzushiwe mambo yakiwamo maradhi makubwa na kashfa
mbalimbali.....
"Sioni
ajabu kuzushiwa mambo ambayo sijayafanya kwani wanamuziki,
wanasiasa na hata viongozi mbalimbali wanakutana na mambo ya
kuzushiwa kwa kuwa wanajua wakifanya hivyo watawaangusha
kutokana na vyeo vyao lakini bado tupo bana," alisema Komba huku akicheka.
Komba aliendelea kuzungumza kuwa mwaka 2015 utakuwa mwisho wake kuimba na anakusudia kuwarithisha vijana wapya....
Mheshimiwa
Komba alihitimisha kwa kusema kuwa katika maisha yake
hafikirii suala la kufa kwani kifo kipo tu hata ukifikiria na
kukaa kuwaza jambo hilo ni kujitafutia mkosi tu katika maisha
yako.
Post a Comment