Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WANAODHALILISHA WATU MITANDAONI KUKIONA

 

index
Mahmoud Ahmad Arusha
MAMLAKA ya mawasiliano nchini ,TCRA, imewaonya wale wote wanaotumia mitando kuchafua na kudhalilisha watu waache mara moja vinginevyo watakabiliwa na mkono wa sheria.
Onyo hilo limetolewa leo(jana) mjini Arusha na kaimu mkurugenzi wa mamlaka ya mawasiliano nchini TCRC, Dkt, Raynold Mtungahema, alipokuwa akitoa ufafanuzi wa maswali ya wanahabari kuhusu kuenea kwa picha chafu zinazowadharirisha watu mbalimbali kwenye mitandao..
Mtungahema, amesema matumizi ya mitandao ambayo sio sahihi ni kosa la jinai na hivyo wale wote wenye tabia hiyo waache mara moja na akawataka  wanaochafuliwa kupitia mitandao wafungue majalada polisi na mamlaka hiyo itasaidia kuwafuatilia wahusika na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria .
Alisema mitandao yote imesajiliwa hata kama aliyehusika kuchafua anaishi uvunguni atakamatwa kwa kuwa mitandao haipo kwa ajili ya matumizi yasiyo sahihi  ambayo hayaruhusiwi.
Mtungahema,  amesema  atakaebainika anatumia mtandao kumchafua mtu mwingine huyo amefanya kosa la jinai hivyo afikishwe mbele ya vyombo vya sheria kwa kuwa tayari zipo sheria zinazotoa adhabu kwa mtuhumiwa atakaepatikana na hatia.
Aliongeza kuwa TCRA, imeshapokea malalamiko mengi na tayari wahusika wameshatiwa mbaloni  na ufuatiliaji utaendelea ili mradi tu mamlaka hiyo itaarifiwe .
 
 
Nchi wanachama wa jumuia  afrika mashariki zimeaanza kikao cha siku nne  mjini Arusaha kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi wa chang moto mbalimbali zinazoikabili sekta ya mawasiliano.
 
Mwenyekiti wa jumuia hiyo ya sekta za mawasiliano, EACO, Dakta   Fracis Wangusi, amesema sekta ya mawasiliano inakabilwa na changamoto mbalimbali ambazo zinakwamisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano kwa haraka.
Wangusi ambae pia ni mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya mawasiliano nchibni Kenya,amezitaja sekta hizo kuwa ni pamoja na kuhama kutoka mtandao wa analojia kwenda digital na  matumizi ya visumbusi kwa ajili ya luninga.
Aliongeza kuwa , sekta ya simu inakabiliwa na changamoto ya kuwepo gharama kubwa za matumizi ya simu, usambazaji barua na vifurushi kunakofanywa namashirika ya posta unaotokana na ukuaji wa mji ambao haujapangiliwa ,matumizi ya  vikwazo vya kuchelewesha huduma ya haraka ya internet .
 
Alisisitiza kuwa ili kupatikana kwa mafanikio hayo ni kuondoa vikwazo na kuhimiza uwekezaji kwenye sekta ya mawasiliano ICT.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top