UMATI WA WAKAZI WA KIJIJI CHA UCHUNGA WAKITAZAMA AJALI YA FUSO
Miili ya marehemu ikiwa katika eneo la dharura katika
hospitali ya mkoa wa shinyanga
Hapa ni katika eneo la dharura katika hospitali ya mkoa wa
Shinyanga ambapo majeruhi 29 hadi sasa wamepokelewa kufuatia ajali ya gari aina
ya fuso iliyokuwa imebeba watu wengi pamoja na mizigo kuelekea katika mnada wa
Mhunze uliopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.Ajali hiyo imetokea asubuhi ya
leo Alhamis.Pichani majeruhi waliendelea kuhudumiwa na wataalam wa afya katika
hospotali ya mkoa wa Shinyanga
|
Kwa
mujibu wa kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dkt Maguja
Daniel ameiambia malunde1 blog kuwa mpaka sasa wamepokea miili miwili ya
marehemu na majeruhi 29 |
|
Huduma inaendelea kutolewa katika hospitali ya mkoa wa
Shinyanga
|
Baadhi ya majeruhi wameiambia blog Hii kuwa gari aina ya
fuso waliyokuwa wamepanda tena kwa kujazana ilikuwa inafukuzana na fuso
nyingine na ghafla walijikuta wakiwa wameshapinduka
|
Kulia ni kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa
Shinyanga Dkt Maguja Daniel akichukua maelezo kutoka kwa askari wa usalama
barabarani
|
Kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dkt
Maguja Daniel akizungumza na waandishi wa habari hivi punde-Picha zote na
Kadama Malunde-Malunde1 blog
Watu
3 wamekufa na wengine zaidi ya 47 wamejeruhiwa baada ya gari walilokuwa
wakisafiria kwenda mnadani kupinduka wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga.
Ajari
hiyo imetokea asubuhi katika eneo la uchunga wilayani humo baada ya
gari hilo haina ya fuso namba T680 ARL kuacha njia na kupinduka.
Chanzo
cha ajari hiyo ni mwendo kasi na derava wa gari hilo aliyetambulika kwa
jina la Shija Ngassa amekimbia baada ya ajari hiyo
Ajari
hiyo ya fuso imesababisha vifo vya watu watatu ambapo moja ametambulika
kwa jina la Difa Shimo mili ya marehemu imehifadhiwa kwenye hospitali
ya mkoa wa Shinyanga.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Shinyanga kamishina msaidizi wa polisi Jastus Kamugisha amethibitisha kutokea kwa ajari hiyo.
Kamugisha
amesema jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo pamoja
na kumsaka dereva wa gari hilo sanajali na kutoa onyo kwa wafanya
biashara wa minadani kuacha kupanda magari ya mizigo
Post a Comment