Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KITU ANACHOKISAKA KWA UDI NA UVUMBA AUNTY EZEKIEL KWA SASA HIKI HAPA ...

MWIGIZAJI nguli katika tasnia ya filamu Bongo, Aunt Ezekiel (pichani) anadaiwa kuanza kusaka mtoto ikiwa ni miaka miwili tangu afunge ndoa na Sunday Dimonte.
 
Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa Aunt, siku si nyingi staa huyo atakwenda kuweka makazi ya muda kwa mumewe Dubai hadi atakapopata ujauzito.
Akizungumza na Amani hivi karibuni, rafiki huyo ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe kwa kuogopa kusutwa na ‘matarumbeta’, alisema wengi wanadai mume wa Aunt yuko jela kwa hiyo ili kuwahakikishia kuwa kitu hicho hakipo ameamua aende kuishi Dubai kwa muda hadi atakaponasa ujauzito.
Aunt Ezekiel

“Kama mipango yake itakwenda vizuri, baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kupita ataondoka na safari hii atakaa sana Dubai hadi Mungu atakapomjalia kupata mimba ndipo atarejea Bongo. Lakini baadaye ataondoka tena kwani hata kujifungua amependa akajifungulie Dubai,” alisema rafiki huyo.
Baada ya kupata nyepesinyepesi hizo, Amani lilimtafuta Aunt na kufanikiwa kukutana naye uso kwa uso alipoulizwa alisema hapendi kuweka hadharani mambo yake na mumewe lakini kuhusiana na ishu ya kwenda kuishi Dubai, muda si mrefu ataondoka.
“Nadhani unajua kuwa mke na mume Mungu akiwajalia afya njema ni muhimu ndoa ijibu kwa kupata mtoto, sasa kuhusu kwenda kuishi Dubai ndiyo mipango yangu.
“Nataka kuwakomesha wale wanaodai kuwa mume wangu amefungwa! Sitaki kuwajibu kwa maneno, nataka kuwajibu kwa vitendo,” alitamba Aunt.
GPL
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top