Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAJINA YA MAJERUHI WA AJALI YA FUSO WALIOHAMISHIWA HOSPITALI YA BUGANDO MWANZA KWA MATIBABU ZAIDI

 



Majeruhi 6 kati ya 35 waliokuwa wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga baada ya kupata ajali wakati wakisafiri na gari aina ya fuso,lililopinduka jana asubuhi katika eneo la Uchunga wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga wamepelekwa katika hospitali ya rufaa jijini Mwanza kwa ajili ya matibabu zaidi.

Majeruhi wengine 11 jana walikimbizwa katika hospitali ya Kolandoto.

Kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dkt Daniel Maguja amewataja waliopelekwa  Bugando  kuwa ni  Masanja Kishiwa 42 mkazi wa Mwajiginya),Mayala Lugomela (31 mkazi wa Jijongo,Malando Mashamindi(20) mkazi wa Nobola,Marco Bundala 19 mkazi wa Jijongo, Jeremia Jisena 35 mkazi wa Mwaweja na Ndila Shigela 41 kutoka kijiji cha Mwajiginya wilayani Kishapu. 

Amewataja waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo kuwa ni ni Charles Makengwa,  Difa Shimo miaka 28 wote wakazi wa wilaya ya Kishapu na kwamba maiti moja ndugu zake bado hawajapatikana ili kuitambua.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top