Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ARSENAL PUNGUFU YAPATA SARE UGENINI LIGI YA MABINGWA

ARSENAL imejiweka katika mazingira mazuri ya kuvuka hatua ya mchujo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, baada ya kulazimisha sare ya bila kufungana na wenyeji Beskitas, Uwanja wa Ataturk. 
The Gunnes walimpoteza nyota wao, Aaron Ramsey aliyeonyeshwa kadi ya pili ya njano na kuwa nyekundu dakika ya 80 baada ya kucheza rafu.
Mkali mpya: Demba Ba (kulia) aliyejiunga na Besiktas kwa Pauni Milioni 4.7 kutoka Chelsea msimu huu leo alikuwa mwiba mbele ya mabeki wa Arsenal
Katika mchezo huo, mshambuliaji wa zamani wa Chelsea, Demba Ba alikaribia kuifungia Beskitas dakika ya sita baada ya shuti lake kugonga besela, wakati Alex Oxlade-Chamberlain naye pia alikaribia kuifungia Arsenal alipogongesha mwamba mwishoni.
Kocha wa Besiktas, Slaven Bilic pia alipandishwa jukwaani mwishoni mwa mchezo. Mchezo wa marudiano utafanyika Jumatano ijayo Uwanja Emirates. 
Kikosi cha Besiktas: Tolga, İsmail, Motta, Ersan, Pedro, Olcay/Tore dk72, Veli, Necip, Ozyakup/Frei dk80, Mustafa/Tosun dk88 na Demba Ba.
Arsenal: Szczesny, Debuchy, Koscielny, Chambers, Monreal, Arteta/Flamini dk50, Ramsey, Cazorla/Rosicky dk90, Wilshere, Sanchez/Oxlade-Chamberlain dk72 na Giroud.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top