Washindi mara tano wa kombe la klabu bingwa barani ulaya Liverpool watakutana mabingwa watetezi wa kombe hilo Real Madrid.
Liverpool
ikiwa imerejea tena kwenye michuano hiyo baada ya kutokuwepo kwa
kipindi cha miaka mitano, pia wako kwenye kundi moja na Basel na
Ludogorets ya Bulgaria.
Manchester City itakutana na Bayern Munich kwa mara ya tatu katika misimu minne,halikadhalika CSKA Moscow itamenyana na Roma.
Arsenal itakabiliana na Borussia Dortmund katika msimu wa pili,nayo Chelsea itamenyana na Schalke,pia Lisbon na Maribor.
Post a Comment