Moses Mashalla,
Mahakama
kuu nchini kitengo cha biashara kanda ya Arusha imemuamuru
mfanyabiashara ambaye pia ni mmiliki wa hoteli ya Snowcrest ya jijini
Arusha,Wilfred Tarimo pamoja na familia yake kumlipa jumla ya $ 1.7 sawa
na zaidi ya sh,3 bilioni mkurugenzi wa kampuni ya Grand Alliance
Ltd,James Ndika kama malipo ya awamu ya kwanza ya kununua hisa ndani ya
hoteli hiyo.Mbali
na agizo hilo mahakama hiyo pia imeagiza washtakiwa wanne kati ya
watano katika kesi hiyo walipe kiasi cha riba cha asilimia 4 ya fedha
hizo tangu kufunguliwa kwa kesi hiyo na kiasi kingine cha asilimia 7
tangu kufungwa kwa shauri hilo hadi siku ya malipo.



Post a Comment