Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mrembo Amwagiwa Mafuta ya Moto Usoni kisa mume wa mtu





Mwanadada aliyefahamika kwa jina moja la Mbuva, mkazi wa Gongo la Mboto jijini Dar, hivi karibuni amejikuta akiharibiwa uso wake kwa kumwagiwa mafuta ya moto na shosti wake aitwaye Mama Sofia, kisa kikidaiwa ni mume wa mtu.




Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo inadaiwa mama Sofia alimfanyia mwenzake unyama huo akimtuhumu kutembea na bwana wake.Akisimulia ilivyokuwa, Mbuva alisema: 

“Mama Sofia alipewa maneno ya uongo kwamba akiwa safarini eti nilitembea na bwana yake.
 
“Siku ya tukio alinipigia simu akaniita kwake, nilikuwa sipajui ila akanielekeza, ile nafika tu majirani zake wakamwambia mimi ndiye nilikuwa nakwenda kulala pale na mume wake.

“Nikajaribu kujitetea lakini hakunielewa. Nikaondoka, baadaye akaniita tena, kufika pale nikakuta ugomvi kati ya mama Sofia na mumewe, ghafla mama Sofia akatoka akiwa na kikombe cha mafuta ya moto akanimwagia usoni.
 
“Nikaanza kupiga kelele, watu wakajaa  ndipo tukachukuliwa wote na kupelekwa katika Kituo cha Polisi cha Mazizini na tukaandikisha, mimi nikakimbizwa hospitali. Ameniharibu uso wangu bila kosa, Mungu atanilipia kwani naamini malipo ni hapahapa duniani.”
 
Mama Sofia hakuweza kupatikama mara moja kuzungumzia tukio hilo.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top