Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishina Msaidizi wa Polisi EMMANUEL G. LUKULA (ACP) akiongea na waandishi wa habari.
*******
Polisi Mkoani Dodoma JANA asubuhi ililazimika kuzifunga baadhi ya barabara za mkoa huo ili kukabiliana na waandamanaji wa CHADEMA waliokuwa wamepanga kuvamia Bunge Maalum la katiba wakitaka Lisitishwe.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishina Msaidizi wa Polisi
EMMANUEL G. LUKULA (ACP) amesema katika hilo kuna gari lenye namba za
usajili T.792 CAX aina ya Pick up Ford Ranger nyeupe mali ya CHADEMA
iliyokuwa ikiendeshwa na CHRISTOPHER NYAMWINJA, Mweneye miaka 52, Mgogo,
Mkristo Mratibu wa CHADEMA Kanda ya magharibi ambapo
makazi yake ni TABORA mjini limekamatwa mtaa wa KUU karibu na kituo cha
mafuta cha GAPCO jirani na WIMPI RESTAURANT likiwa na watu wengine
watatu ambao ni:-
Aidha Kamanda LUKULA – ACP ameongeza kuwa kabla ya kukamatwa kwa gari hilo Polisi walilikimbiza na katika kupita kwenye kona/mtaa watu wawili waliruka kutoka kwenye gari hilo na kukimbia kusikojulikana na bango hilo. Watu waliobaki ndani ya gari hilo ambao ni wanne ndio waliokamatwa.
- LAURENT S/O MANGWESHI mwenye miaka 36, Mkristo, Msukuma Mkulima wa Wialya ya Mpanda Mkoa wa Katavi.
- AGNES D/O STEPHANO mwenye miaka 26, Mhehe, Mkristo Mfanyabiashara Mkazi Ubungo Maziwa Dar es Salaam.
- ELISHA S/O DAUDI mwenye miaka 49, Msukuma, Mkristo Fundi umeme Mkazi wa TAbora.
Aidha Kamanda LUKULA – ACP ameongeza kuwa kabla ya kukamatwa kwa gari hilo Polisi walilikimbiza na katika kupita kwenye kona/mtaa watu wawili waliruka kutoka kwenye gari hilo na kukimbia kusikojulikana na bango hilo. Watu waliobaki ndani ya gari hilo ambao ni wanne ndio waliokamatwa.
Askari Polisi wakiwa katika ulinzi kudhibiti maandamano.
Jeshi la polisi limeimalisha ulinzi katika maeneo yote ambayo yalitajwa na chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwa ndiyo watapitia wakiandamana kwenda kwenda Bungeni kuanzia saa 4 asubuhi ya JANA.
Polisi wakiwa wamefunga kamba kati barabara ya mzunguko ya stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani na chuo cha biashara CBE kwaajili ya kuwazuia waandamanaji hao waliopanga kwenda Bungeni.
Polisi wapanda farasi wakiimalisha ulinzi katika viwanja vya nyerere Squere ambapo Chadema wamepanga kuanzia maandamano kuelekea bungeni.
Askali polisi wakiwafanya mawasiliano kwenye gari lao ambalo lilikuwa limepakia mbwa kwa ajili ya kuimalisha ulinzi katika viwanja vya Nyerere Dodoma kwa ajili ya kuwazuia waandamanaji wa Chadema walipanga kuandamana kwenda Bungeni.
Post a Comment