Meneja
wa Shirika la Nyumba mkoa wa Pwani Pauline Mrango akisoma Hotuba ya
makabidhiano ya mashine 28 za kufyatulia matofali kwa vikundi vya vijana
katika halmashauri zote za mkoa wa Pwani.
Shirika
la Nyumba la Taifa limetoa mashine hizo zenye gharama ya zaidi ya
shilingi milioni 12 pamoja na mafunzo kwa vijana ya wiki mbili ambapo
baada ya kumaliza mafunzo Shirika litatoa msaada wa shilingi laki tano
kwa kila kikundi kama mtaji .
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimpa mkono wa pongezi Meneja wa
Shirika la Nyumba la Taifa mkoa wa pwani Pauline Mrango kwa kutoa
mashine 28 za kuwasaidia vijana.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuashiria
makabidhiano ya mashine za kufyatulia matofali zilizotolewa na shirika
la nyumba la Taifa kwenda kwenye halmashauri zote za mkoa wa Pwani.
Mashine 28 zitawasaidia vijana mkoa wa Pwani kuondokana na tatizo la
ajira, pili litasaidia sana katika utunzaji wa mazingira,zitasaidia
wananchi kujenga nyumba za kisasa na kwa bei nafuu.(Adam Mzee)
Post a Comment