Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS JAKAYA KIKWETE RAIS KIKWETE AFANYA UTEUZI WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Rais Jakaya Kikwete amemteua Bw. Seperatus R. Fella kuwa  Katibu wa Sekretarieti ya Kamati ya Kuzuia Biashara Haramu ya Binadamu.

Kabla ya uteuzi huo, Bw. Fella alikuwa Kaimu Katibu wa Kamati hiyo  na uteuzi wake unaanzia mwezi Agosti, 2014.

Kamati ya Kuzuia Biashara Haramu ya Binadamu ilianzishwa chini ya Sheria ya Kuzuia Biashara Haramu ya Binadamu ya mwaka 2008 na kazi kubwa ya Kamati hii ni  kuzuia na kudhibiti biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu.

Chimbuko la kutungwa kwa Sheria ya Kuzuia Biashara haramu ya Usafirishaji wa Binadamu ni Itifaki ya Kimataifa ya kuzuia, kupambana na kutoa adhabu kwa watekelezaji wa biashara ya usafirishaji haramu ya binadamu, hasa wanawake na watoto.

Itifaki hii ni nyongeza ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa dhidi ya uhalifu wa kimataifa wa kupangwa, ambapo Serikali ya Tanzania imeridhia Mkataba huo na itifaki yake.

Juhudi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania za kushughulikia biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu zinaendana  pia na Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu, Mkataba wa Kimataifa wa kuondoa aina zote za ubaguzi dhidi ya Wanawake na Mkataba wa Haki za Watoto wa mwaka 1989.

Makosa yanayovunja Sheria ya kuzuia Usafirishaji haramu wa Binadamu ni pamoja na kupanga, kupangisha au kutumia nyumba au jengo kwa ajili ya biashara ya usafirishaji wa binadamu na kughushi hati za Serikali kwa madhumuni ya kukuza biashara ya binadamu.  

Makosa mengine ni kujipatia pesa kwa kuwatumikisha kwa nguvu watu wazima au watoto wa kike au kiume katika kufanya kazi za ndani au biashara nyingine haramu kama ngono na usafirishaji na usambazaji wa madawa ya kulevya, baada ya kuwalaghai au kuwachukua kwa nguvu kutoka katika makazi yao.
 

Adhabu kwa wanaotiwa hatiani kwa kuvunja Sheria hii ni kifungo kisichopungua mwaka mmoja (1) au kisichozidi miaka saba (7) au faini isiyopungua shilingi milioni mbili (2) au kuzidi milioni 50 au vyote kwa pamoja.

Imetolewa na:

Isaac J. Nantanga

MSEMAJI

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

23 OKTOBA, 2014
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top