Zaidi ya wakazi 200 katika kijiji kimoja kaskazini mwa India wamehudhuria sherehe ya harusi ya nyani wawili.
Sherehe
hiyo ilifanyika siku ya Jumatatu katika wilaya ya Bettiah, katika jimbo
la Bihar, huku "bi harusi" akiwa amevalia gauni maridadi.
Nyani ni viumbe wanaopendwa na watu wa jamii ya wa-Hindu.
"Bwana
harusi" ambaye anajulikana kama Ramu pamoja na mkewe mpya aitwaye
Ramdulari walipitishwa katika mitaa ya kijiji wakiwa juu ya gari
lililopambwa kwa maua na muziki ukichezwa, huku mamia ya wanakijiji
wakijipanga kuwashangilia.

Mmiliki wa nyani hao Udesh Mahto ambaye ana watoto watatu wa kiume amesema nyani Ramu ni kama mtoto wake wa kwanza.
"Nilitaka yeye ndio aanze kuoa," ameiambia Idhaa ya BBC ya Kihindi.
Bwana Mahto alimnunua Ramu kutoka Nepal miaka saba iliyopita, na baadaye kumnunua Ramdulari katika soko la kijiji.


Post a Comment