Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

HARUSI YA NYANI INDIA YATIA FORA

Zaidi ya wakazi 200 katika kijiji kimoja kaskazini mwa India wamehudhuria sherehe ya harusi ya nyani wawili. 
Harusi hiyo iliandaliwa na mmiliki wa nyani hao, ambaye alisema nyani dume ni kama "mwanaye".
Sherehe hiyo ilifanyika siku ya Jumatatu katika wilaya ya Bettiah, katika jimbo la Bihar, huku "bi harusi" akiwa amevalia gauni maridadi. 
Nyani ni viumbe wanaopendwa na watu wa jamii ya wa-Hindu.
"Bwana harusi" ambaye anajulikana kama Ramu pamoja na mkewe mpya aitwaye Ramdulari walipitishwa katika mitaa ya kijiji wakiwa juu ya gari lililopambwa kwa maua na muziki ukichezwa, huku mamia ya wanakijiji wakijipanga kuwashangilia.
Mmiliki wa nyani hao Udesh Mahto ambaye ana watoto watatu wa kiume amesema nyani Ramu ni kama mtoto wake wa kwanza.
"Nilitaka yeye ndio aanze kuoa," ameiambia Idhaa ya BBC ya Kihindi.
Bwana Mahto alimnunua Ramu kutoka Nepal miaka saba iliyopita, na baadaye kumnunua Ramdulari katika soko la kijiji.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top