Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA NA UJUMBE WAKE AWASILI MKOANI DODOMA KUANZA ZIARA YA SIKU TISA


 Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa uwanja wa ndege mjini Dodoma mapema leo asubuhi na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa huo, Mh. Adam Kimbisa,tayari kwa kuanza ziara ya siku tisa, yenye lengo la kukagua, kuhimiza miradi ya maendeleo ya wananchi pamoja na kuangalia uhai wa chama, ambapo mara baada ya kuwasili amefanya mkutano wa ndani na Wajumbe wa Halmashauri kuu ya Wilaya ya Mpwapwa yenye majimbo mawili ya Uchaguzi.Kinana ametokea Mkoani Ruvuma mara baada ya kushiriki mazishi ya aliekuwa Mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi,Marehemu Kapteni John Komba aliyezikwa kijijini kwao Lituhi.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akilakiwa na Mkuu wa Mkoa Dodoma,Mh.Chiku Galawa mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege mkoani Dodoma mapema leo asubuhi,kulia kwake ni  Katibu wa CCM Mkoa,Albert Mgumba
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Taifa,Nape Nnauye akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mh.Chiku Galawa mapema leo asubuhi mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege,tayari kwa kuanza ziara ya siku 9 mkoani humo,
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa,Mh.Addam Kimbisa akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Ujumbe wake pamoja na baadhi ya Wananchi (hawapo pichani) mara baada ya kuwasili katika ofisi za CCM Wilaya ya Mpwapa mapema leo asubuhi.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza na baadhi ya Wanachama wa CCM waliofika mapema leo katika ofisi za CCM wilaya ya Mpwapwa kumpokea Ndugu Kinana na Ujumbe wake,ambapo anaanza rasmi ziara yake wilayani humu na vitongoji vyake.
PICHA NA MICHUZIJR-MPWAPWA.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top