Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Diamond: Hakuna msanii ambaye nimewahi kumlipa wala yeye kunilipa kufanya collabo



Diamond Platnumz amesema kuwa ameshafanya collabo na wasanii A-list karibu wote wanaofanya vizuri Afrika, lakini hakuna hata mmoja ambaye amewahi kumlipa wala wao kumlipa kwaajili ya collabo hizo.

“Nimefanya collabo na wasanii tofauti tofauti, karibuni A-list wote ya wanaofanya vizuri Afrika nimeshafanya nao.” Alisema kupitia XXL ya Clouds Fm.
 
Ameongeza kuwa mwanzoni haikuwa rahisi kufanya nao kutokana na kwamba wengi walikuwa hawamfahamu tofauti na ilivyo sasa.
 
“Kiukweli sijawahi kufanya malipo ya mtu yoyote kufanya naye nyimbo. Mwanzoni wakati naanza kufanya ilikuwa kidogo tabu kwasababu mtu alikuwa hajafahamu anafanya nyimbo na nani, lakini sasa hivi wanafahamu kwamba…nikifanya nyimbo na Diamond, East Afrika mimi kwangu inakuwa kiurahisi nyimbo yangu, na upande wangu mimi inakuwa ni rahisi kwa West, kwahiyo tukichanganya inakuwa rahisi zaidi. 
 
"Kwahiyo hakuna mtu ambaye nimeshawahi kumlipa wala yeye mimi kunilipa hii ni uongo sijawahi kufanya hivyo.”
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top