Yafuatayo ni maneno kwenye mistari tofauti iliyoandikwa na Rais
Jakaya Kikwete ikiwa ni miezi mitatu tu imebaki Tanzania kuingia kwenye
uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge.
Hii ni tweet ya kwanza aliandika July 4 2015 >>> ‘Utaratibu
bora wa kuchagua kiongozi wa nchi si wa kuanza kujadili majina, bali wa
kuanza kujadili changamoto na vipaumbele vya Taifa kwanza‘
Tweet alizoandika July 5 2015 >>> ‘Tusiwasikilize
wanasiasa wanaowagawa Watanzania na kutumia fedha kutafuta madaraka.
Mchezo wao ni mauti yetu. Wakatalieni kwa macho makavu, Tusiruhusu
wanasiasa kutumia dini ambazo ni mhimili muhimu wa amani yetu. Ukiwepo
mfarakano wa kidini hakuna mtu wala eneo litakalonusurika’
Mstari mwingine ameandika >>> ‘Tukiamua
kwa utashi wetu kuzipoteza tunu za amani na upendo, katu hatuwezi
kusema ni mapenzi ya Mungu bali itakuwa ni makosa yetu wenyewe, kiongozi
wa dini anapaswa kukumbusha wajibu wa: kujiandikisha, kupiga kura na
kuchagua kiongozi bora; si kuwaambia waumini wamchague fulani‘
Post a Comment