Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MTANGAZA NIA UBUNGE LUDEWA AANGUKIA PUA



Aliyeshindwa ujumbe wa NEC Ludewa Injinia Zephania Chaula  akiangana na mbunge  Deo  Filikunjombe baada ya  kushindwa katika nafasi  hiyo ,Chaula alikuwa ni mmoja wa wana CCM waliokuwa  wakitaka kuwania ubunge jimbo la Ludewa


Chaula akiagana na mshindi mzee Nkwera 
 Mkuu  wa wilaya ya  Ludewa Antonia Choya akimkabidhi  hati ya  shukrani mbunge wa Ludewa  Deo Filikunjombe (kushoto)
 Mjumbe  wa  mkutano huo Bw  Choya  akipiga  kura.
 Wajumbe  wakishiriki  kupiga  kura.
 Wajumbe  wakishiriki  kupiga kura
 Mgombe  Chaula  akishukuru kwa  kushindwa
 Injinia  Chaula  akimpongeza mshindi mzee Nkwera.
Mbunge  wa  jimbo la  Ludewa  Deo Filikunjombe  akipiga  kura  kumchangua mjumbe wa NEC Ludewa
MBIO za  ubunge jimbo la  Ludewa  mkoani  Njombe zimeishia hewani  kwa mtangaza  nia wa  wanafasi hiyo Injinia  Zephania  Chaula  baada ya kuambilia  kura 11 pekee katika nafasi ya mjumbe  wa Halmashauri  kuu ( NEC) Taifa kutoka  wilaya ya Ludewa  aliyokuwa akiwania dhidi ya katibu msaidizi  wa mbunge wa  jimbo la Ludewa  Hilaly  Nkwera  aliyeibuka mshindi kwa  kupata  kura 138 kati ya  kura  zote halali 151 zilizopigwa .
Huku mgombea  huyo aliyeshindwa katika nafasi hiyo ya Ujumbe wa NEC Injinia Chaula  akiapa  kutogombea tena nafasi hiyo kwa madai kuwa ni mara ya pili sasa anashindwa  vibaya  katika  mchakato 
wa  kuwania nafasi hiyo ambapo awali alishindwa mgombea  wa darasa  la  saba marehemu Elizabeth Haule .
Uchaguzi huo  mdogo  wa  kuziba nafasi ya  mjumbe  wa  NEC  iliyoachwa  wazi na aliyekuwa  mjumbe wa nafasi hiyo Elizabeth Haule  aliyefariki  dunia mapema mwaka  huu ,ulifanyika  mwishoni mwa  wiki  hii kwa kuwashirikisha  wagombea  hao  wawili kabla ya mgombea  mwingine ambae ni mbunge  wa  jimbo la Ludewa Deo  Filikunjombe  kuandika barua ya kujitoa katika  kinyang’anyiro  hicho akiwapisha wagombea  hao wachuane  kutokana na yeye  kudai  kuwa atachukua fomu ya kugombea tena ubunge  wa  jimbo  hilo la Ludewa .

Akitangaza matokeo  hayo ya  uchaguzi msimamizi  mkuu  wa uchaguzi huo  Lucas Nyanda  ambae ni katibu  wa  jumuiya  ya  wazizi wa CCM mkoa  wa Njombe ,alisema  kuwa  jumla ya  wajumbe  waliopaswa  kushiriki katika uchaguzi  huo ni 164 ila   wajumbe  halali  walioshiriki ni 151 na kati ya  wajumbe  hao kura 2  ziliharibika  huku Injinia Chaula akipata  kura 11 na mshindi wa nafasi hiyo Bw  Nkwera  akipata  kura 138
Awali mbunge  wa  jimbo la  Ludewa  Bw  Filikunjombe  ambae alikuwa ni mmoja kati ya  wana CCM watatu  ambao majina  yao yalirejeshwa  kuwania nafasai hiyo alisema  kuwa analazimika  kujitoa katika  nafasi hiyo ili  kupisha wanachama  hao wawili  ambao wamemzidi  umri  ili  kuweza kupambana  na  yeye ataendelea  kuwa kuwatumikia  wananchi  wa Ludewa katika nafasi ya  ubunge pekee.
Akiwashukuru wajumbe kwa ushindi  huo  wa nafasi ya ujumbe wa NEC Bw  Nkwera ambae kitaaluma ni mwalimu na pia amepata  kuwa mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa na mwenyekiti wa madiwani wa mkoa wa Njombe na Iringa alisema kuwa amefurahishwa na imani  kubwa ambayo wana CCM wameionyesha  kwake  kwa kumchagua  kuwa mwakilishi wao katika vikao  vya  kitaifa .
Bw Nkwera  alisema wana CCM Ludewa waamini  kuwa nafasi hiyo hawajakosea kumpa na kamwe hatawaangusha kwani atahakikisha anawatumikia  vema katika vikao  vya  juu kwa kuanza na  safari ya kumpata mgombea wa nafasi ya  Urais wa CCM ambae atakuwa ni chaguo la  wana CCM wote wa Ludewa .
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top