Wizara
ya Afya na Ustawi wa Jamii nchini imesema watu 7 wamekufa kwa ugonjwa
wa kipindupindu huku wagonjwa 230 wakilazwa katika kambi mbali mbali
maalum katika mikoa ya Dar es Salaam na Morogoro.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Waziri wa Afya na
Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashid amesema kuwa kati ya wagonjwa hao 194
ni kutoka Dar es Salaam na 36 ni kutoka Mkoa wa Morogoro.



Post a Comment