Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SOMA HAPA HOTUBA KAMILI YA DR. SLAA .... AFUNGUKA MENGI MAZITO


Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Dk. Wilbroad Slaa pia amesema kuwa mambo yaliyotokea katika chama chake ndio maana ameamua kuachana na siasa  rasmi hii leo.


 1.Napenda  kumshukuru  mwenyezi  mungu  kwa  kutujalia  uzima.

2. Nimeamua  kujitokeza  leo  hii  ili  kukomesha  upotoshaji  na  kuuweka  wazi  ukweli.


3.Sina  tabia  ya  kuyumbishwa  na  ninasimamia  ninachokiamini.

4.Sina  ugomvi  na  kiongozi  yeyote  maana  siasa  sio  uadui.

5. Siasa  inapoongozwa  kwa  misingi  ya  upotoshaji, matokeo  yake  ni  vurugu.

6. Naweka  wazi  kuwa  mimi  sikuwa  likizo  na  hakuna  mtu  yoyote  aliyenipa  likizo.

7.Kilichotokea  ni  kuwa  niliamua  kuachana  na  siasa  tangu  tarehe  28.7.2015  saa  sita  usiku  baada  ya  kutoridhishwa  na  kilichokuwa  kinaendelea  ndani  ya  chama  changu.

8.Ni  kweli  nilishiriki  kumleta  Lowassa  CHADEMA  Lakini  nilikuwa  na  misimamo  yangu  ambayo  ilitufanya  tusielewane. 

9. Baada  ya  Lowassa  kukatwa  pale  Dodoma, Gwajima  ambaye  ni  mshenga  wa  Lowassa  alinipigia  simu  kutaka  kujua  ninii  cha  kufanya.

10. Nilimpigia   Mwenyekiti    Mbowe  kumjulisha  na  tukakubaliana  kupanga  muda  wa  kuwasikiliza.

11. Kabla  ya  kuanza  kuwasikiliza, msimamo  wangu  ulikuwa  ni  kumtaka  Lowassa  kwanza  atangaze  kuhama  chama, aweke  wazi  ni  chama  gani  anaenda  na  ajisafishe  juu  ya  tuhuma  zake

12.Tangu  akatwe  jina, Lowassa  hakutangaza  kujitoa  CCM  na  wala  hakujisafisha  na  tuhuma  zake, kitu  kilichonifanya  nitofautiane  naye.

13. Niliwauliza  wanachadema  wenzangu  kuwa  Lowassa  anakuja  kama  Mtaji  au  Mzigo?

14. Swala  sio  urais  kama  watu  wanavyozusha, mimi  nilikuwa  nataka  mgombea  mwenye  uwezo  na  sifa  ambaye  ataweza  kuitoa  CCM.  Sikuwa  na  tamaa  ya  urais  kama  watu  wanavyosema 

15. Tangu  Gwajima  atupe  taarifa  za  ujio  wa  Lowassa, Swali  langu  la  Lowassa  kuwa  Mtaji  au  mzigo  halikuwahi  kujibiwa.

16. Nilitaka  kujua  ni  mtaji  gani  lowassa  atakuja  nao  na  ni  viongozi  gan  atakuja  nao.

17. Nilijibiwa  kuwa  anakuja  na  wabunge  50  wa  CCM, wenyeviti  22  wa  mikoa  na  wenyeviti  80  wa  wilaya.

18.Baada  ya  ahadi  hiyo, nilitaka  sasa  nipewe  majina  ya  hawa  watu  lakini  mpaka  tarehe  25  july  sikupewa  hayo  majina 

19. Wenzangu  waliniambia  kuwa  tarehe  27  niitishe  kikao  cha  dharura  ila  niligoma  kwa  sababu  nilikuwa  sijapewa  haya  majina 

20. Ndani  ya  kikao  hicho,  tulianza  kwa  mabishano  makali  kati  yangu  na  Mbowe, Lissu  na  Gwajima, viongozi  wenzangu  ni  shahidi  na  mungu  anajua. Msimamo  wangu  ulikuwa  ni  uleule  kujua  mchango  wa  Lowassa 

21. Kikao  kile  kikavunjika, baadae  tukaingia  kamati  kuu  lakini  bado  msimamo  wangu  ulikuwa  ni  uleule. Baadae  nikaandika  barua  ya  kujiuzulu.

22.Profesa  Safari  aliichana  ile  barua. 

23.Cha  kusikitisha  ni  kuwa  Kesho  yake  picha  zikaanza  kusambaa  mtandaoni  zikimuonyesha  na  lowassa  japo  viongozi  wangu  walizikana  zile  picha.  Kibaya  ni  kuwa  viongozi  waliuficha  ukweli 

24.  Kesho  yake  niliandika  tena  barua  rasmi  ya  kujiuzulu. 

25. Baada  ya  pale  zikaanza  propaganda  za  uongo  zikimuhusisha  hadi  mke  wangu  eti  kanizuia.

26. Naomba  watanzania  wajue  kuwa  mke  wangu  hakuwahi  kunizuia  kwa  lolote, lkn  hata  angefanya  hivyo  sio  mbaya  maana  hata  yeye  ni  mwanaharakati  mwenye  uchungu  na  nchi  hii. 

27. Mke  wangu  aliwahi  hadi  kuumia  wakati  akipigania  ukombozi  wa  nchi  hii.....Lakini  sio  mbaya, familia  yangu  imezoea  propaganda. 

28. Kikubwa  katika  harakati  ni  credibility  ambayo  lazima  uilinde  na  mimi  sitaki  jina  langu  liharibiwe  na  ni  haki  yangu.

29. Maslah  mapana  ya  taifa  ndiyo  yaliyotufikisha  hapa  na  sio  maslahi  binafsi. 

30.Lowassa  na  wapambe  wake  ni  waongo  maana  hakuna  hata  kipengele  kimoja  walichokitekeleza.

31. Tulitaka  hao  wabunge  50  waje  kwanza  kabla  ya  mchakato  wa  uteuzi  ccm

32. Napinga  kuchukua  makapi  ya  CCM  na  kuyaita  MTAJI.

33.Mtu  kama  Sumaye  ni  FISADI  na  nilikuwa  siongei  naye 

34. Sumaye  aliwahi  kusema  CCM  wakimchagua  Lowassa  atahama  chama. Leo  Lowassa  kawaje  msafi?? 

35. Tulitaka  Mtaji  toka  kwa  Lowassa  na  sio  MAKAPI 

36. Wenyeviti  walioletwa  na  Lowassa  ni  MIZIGO  na  namjua  vizuri. Akithubutu  kunijibu  ntamwaga  UOZO  wake  wote 

37.Nani  asiyejua  Guninita  pia  ni  mzigo??

38:  Nawataka  viongozi  wangu  wanijibu  ni  mtaji  upi  walioupata  toka  kwa  Lowassa.

39. Mimi  ni  Padri  Mstaafu, sipendi  siasa  za  uongo. 

39. Ukisema  unataka  kuiondoa  CCM  ni  lazima  ujikumbushe  misingi  ya  CHADEMA  ambayo  ilikuwa  ni  uadilifu. Leo  chadema  hii  ina  Uadilifu  gani?? 

40.  Namshangaa  sana  Lowassa  eti  kusimama  mbele  ya  watu  akijinasibu  kuwa  ni  msafi.....kwamba  mwenye  ushahidi  aende  Mahakamani. Ni  dhambi  kupotosha  watu.

41. CCM    hawana  ujasiri, ni  waoga  na  ndiyo  maana  wamewalea  watu  kama  akina  Lowassa 

42. Ukitoa  kinyesi  chooni  na  kukipeleka  Chumbani  maana  yake  hata  chumba  chako  ni  CHOO  na  kitakuwa  kinanuka  zaidi  kuliko  choo  cha  kawaida 

43.Mimi  nilikuwepo  wakati  sakata  la  Richmond  likijadiliwa.Mimi  nina  ugomvi  wa  muda  mrefu  na  Lowassa.

44.  Mwaka  2010  mimi  nilimtaka  Lowassa  atangaze  Richmond  ni  ya  nani.

45. Leo  tena  namtaka  Lowassa   Lowassa  atoke  hadharani  atangaze  Richmond  ni  ya  nani.  Unaposema  ni  ya  mkubwa, atuambie  mkubwa  gani

46. Ukitaka  kuijua  Richmond  rejea  Ripoti  ya  Mwakyembe. Nampongeza  Mwakyembe  na  Sitta  kujitokeza  hadharan  kuusema  ukweli.

47. Siku  moja  kabla  ya  ripoti  kusomwa, nililetewa  Rushwa  ya  milioni  500  ili  tukaupindishe  ukweli  bungeni  lakini  nilikataa 

48. Ripoti  ya  mwakyembe  iliamua   mambo  mawili,  moja; Lowassa  ajipime  au  bunge  lijadili  na  lichukue  hatua.  Lowassa  kuona  hivyo  akaamua  kukimbilia  kujiuzulu  kukwepa  aibu  ya  kung'olewa  na  bunge 

49:  Lowassa  haaminiki, ni  muongo  na  hastahili  kuwa  Rais  wa  nchi....

50.  Lowassa  ni  FISADI  na  kama  mimi  ni  muongo  ajitokeze  hadharani  akanushe

51. Anasema  Lowassa  ataleta  maji, mbona  jimbo  lake  la  Monduli  halina  Maji???

52.  Mnasema  Lowassa  kaanzisha  shule  za  kata, iv  mjua  msingi  wa  shule  za  kata?  waandishi  rudini  shule  mkajifunze  upya.

53.Nilifanikiwa  kuijenga  Chadema  na  ikawa  tumaini  jipya  la  watanzania.....Vijana  wangu  wa  Chadema, naomba  niwe  mkweli  propaganda  imekivamia  chama.

54.  Inasikitisha  kuona  CHADEMA  inajazwa kwa mabasi  pale  jangwani .....alafu  mnawadanganya  watu  eti  ni   MAFURIKO

55.  CHADEMA  ya  kipindi  changu  ilikuwa  inakemea  Rushwa. Niambien  leo  chadema  watasema  nini  kwenye  majukwaa? 

56. Mnaomtetea  Lowassa  na  nyie  jitokezen  hadharani...mimi  nasema  kwa  sababu  nina  ushahidi  na  sio  lazima  ushahidi  huu  niupeleke  mahakamani.

57. Wenye  uwezo  wa  kumpeleka  Lowassa  Mahakamani  ni  Serikali, na  mwakyembe  alisema  juzi  kuwa  kesi  ya  jinai  haina  kikomo, mtu  anaweza  kushitakiwa  muda  wowote 

58. Sitaki  kuingila  swala  la  Babu  Seya, lakini  waliolawitiwa  ni  watoto  waliokuwa  chini  ya  umri. kwa  nini  haki  yao  ipotee?

59.  Rais  hana  mamlaka  ya  kumtoa  Babu  Seya. Lowassa  asiwadanganye.

60.  Kuhusu  swala  la  Masheikh, Sumaye  ndiye  aliyeamuru  mapolisi  wavamie  misikiti  wakiwa  na  mbwa......Watanzania  msikubali  kudanganywa. hizo  ni  propaganda  za  wasaka  urais 

61. Masikubali  Rais  Muongo  na  mimi  naapa  ntapiga  kelele  kila  kona  kumpinga  Lowassa.

62.Lowassa  alipokuwa  waziri  mkuu, matatizo  yanayotokea  leo  hayakuwepo?  mapigano  ya  wakulima  na  wafugaji  hayakuwepo?

63.  Lowassa  akiwa  waziri  mkuu  alisababisha  migogoro  mizito  sana  kati  ya  monduli  na  karatu.  Rais  wa  aina  hii  wa  nini?

64.  Naomba  nisiongee  mengi  kwa  sababu  ntakosa  ya  kusema  siku  nyingine.....Nawataka  Lowassa  na  Sumaye  wajitokeze  kunijibu.

65. Siku  nyingine  ntakuja  kuongelea  kuhusu  hisa  za  Lowassa  kwenye  makampuni 

66.  Nahitimisha  kwa  kusema  kuwa  Nimestaafu  siasa  na  sina  chama  lakini  nina  nchi, hivyo  ntaendelea  kuwatumikia  watanzania  kwa  jinsi  mungu  alivyonipa  vipawa 


67.  Narudia  tena, Sina  chama  na  sitajiunga  na  chama  chochote. 

Waandishi  wanauliza  Maswali: 
Mwandishi:  Umesema  hujiungi  na  chama  chochote, utawasaidiaje  watanzania?  Rais  gani  unamuunga  mkono?

Mwandishi  Guardian:  Ulisema  Lowassa  atakuwa  assert  kama  atakuja  na  wabunge  na  hao  wenyeviti.  Je  angekuja  kama  assert  ungeyasema  haya  yote?

Mwandishi  binafsi:  Umesema  waliohamia  Chadema  ni  makapi.  Mwaka  1995  Uliihama  CCM,   ukahamia  chadema. Je  na  wewe  ni  KAPI?

Mwandishi-Azam:  Umetangaza  kustaafu  siasa, lakini  bado  unakadi  ya  CCM  na  CHADEMA?  Je  utazirudisha?

Mwandishi  Blog:  Inaonekana  baada  ya  chedema  kukutosa  ndo  maana  unamshambulia  Lowassa, je  ni  kweli?

Majibu:
1. Kadi  ni  mali  zangu  na  siwezi  kuzirudisha. Ya  chadema  nimeilipia  miaka  20,ya  CCM  bado  haijaisha  muda  wake.

2. Kuhusu  urais, mimi  sijagombea  urais  na  sikuchukua  fomu.  sasa  kwa  nini  nikasirike  kisa  wamempa  Lowassa?
Sina  ugomvi  na  Mbowe  na  nakumbuka  alinisaidia  nyumba

3.  Mimi  sio  KAPI....Ili  kuujua  ukweli  unahitaji  kutumia  kigezo. KAPI  ni  yule  aliyekataliwa  na  chama  flani, mimi  sikuwahi  kukataliwa.  Sikuwa  na  uchafu  wowote  wakati  naingia  CCM.

4.  Lowassa  ni  mzigo  tu  hata  kama  angetuletea  hao  watu  wake.....Lowassa  ana  makandokando  mengi. Angetuletea  hao  watu  ndo  tungeamua  tumpokee  au  tusimpokee

5.Mimi  sina  chama  na  sitampigia  kampeni  mtu  yeyote. Mimi  nimefanya  utafiti  kwa Lowassa  pekee, kwamba  taifa  litapata  madhara  gan  Lowassa  akiwa  Rais.....Lowassa  ni  Fisadi.
 
 -Kazi  yangu  leo  ilikuwa  ni  kuwaambia  watanzania  waachanane  na  ushabiki.Ukihamishia  CHOO  chumbani, manake  harufu  itahamia  huko.
 -Chadema  ya  leo  kwa  sasa  imetekwa  na  Lowassa  na  hawawezi  tena  kuongelea  Ufisadi 

Maswali  ya  nyongeza

1.Umesema  waliohamia  chadema  kwa  sasa  ni  sawa  na  mfano  wa  Choo. Je, wewe  ulipohama  hukuwa  choo?  kwa  nini  wewe  uliweza  kukibadili  chama  halafu  akina  Lowassa  washindwe?

Jibu:  Wakati  mimi  nahama  sikuwa  mchafu  kama  hawa  akina  Lowassa  na  Sumaye.



Slaa: Watanzania wana kiu ya kujua kwanini amekuwa kimya kwa muda mrefu sasa licha ya harakati za kisiasa kuendelea.
Muda utakaotumika ni saa moja, hakuna muda mrefu sana.
Ameamua kufanya hayo kwa kuwa imefika mahali ukweli lazima usemwe na upotoshwaji ukomeshwa. Namna pekee ya kufanya hivyo ni kutoka hadharani na kuusema ukweli.
Sote tunafahamu kuwa hana tabia ya kuchenga mambo, mengi yamesemwa na watu tofauti, kwenye mitandao, magazeti na viongozi wake!
Hana ugomvi na kiongozi yoyote, kwa kuwa siasa sio ugomvi. Kama binadamu wa kawaida hana chuki wala hasira na binadamu mwingine yoyote!
Iwe wazi kuwa katika Taifa kuna misingi ambayo inaongoza taifa. Inapofika mahali taifa linaongozwa kwa msingi ya propaganda na upotoshwaji matokeo yake ni vurugu kubwa katika taifa. Yeye amekataa hayo yote!
Anasema kuwa YEYE hakuwa likizo kama inavyosemwa na viongozi wake! Atafafanua kwa kifupi!
Kilichotokea ni kuwa aliamua kuachana na siasa, tarehe 28 Julai 2015, majira ya saa tatu usiku, baada ya kuona yanayofanyika ndani ya chama chake hayamridhishi.


Mtangulizi wa shuguli ambaye anatoka kwenye kampuni ya mahusiano ya umma anamtambulisha Dr. Willibrod Slaa.

Anasema kuwa kwa muda mrefu Slaa amekuwa alama ya harakati za ukombozi dhidi ya makucha ya mkoloni mweusi.

anaongeza kuwa Dr. ataongea kwa muda kisha kuruhusu maswali kutoka kwa waandishi, anamkaribisha!

Kinachosemwa ni kuwa Dr. Slaa alishiriki tangu mwanzo kwenye mchakato. Anasema ni kweli alishirii kwenye majadiliano, akaweka msingi na msimamo wako. Kuna wakati wengi wanashinda kutokana na wingi wao, wewe unayeamini katika misingi inabidi uachie ngazi.

Azam TV wameanza matangazo kupitia kipindi chao cha KITUO CHAKO CHA UCHAGUZI, wako LIVE sasa... Bado uchambuzi wa safari ya Kisiasa ya Dr. Willibrod Slaa unaendelea.

Tumepelekwa moja kwa moja kutoka Hoteli ya Serena

Mtangulizi wa shuguli ambaye anatoka kwenye kampuni ya mahusiano ya umma anamtambulisha Dr. Willibrod Slaa.

Anasema kuwa kwa muda mrefu Slaa amekuwa alama ya harakati za ukombozi dhidi ya makucha ya mkoloni mweusi.

anaongeza kuwa Dr. ataongea kwa muda kisha kuruhusu maswali kutoka kwa waandishi, anamkaribisha!

==========================

Slaa: Watanzania wana kiu ya kujua kwanini amekuwa kimya kwa muda mrefu sasa licha ya harakati za kisiasa kuendelea.

Muda utakaotumika ni saa moja, hakuna muda mrefu sana.

Ameamua kufanya hayo kwa kuwa imefika mahali ukweli lazima usemwe na upotoshwaji ukomeshwa. Namna pekee ya kufanya hivyo ni kutoka hadharani na kuusema ukweli.

Sote tunafahamu kuwa hana tabia ya kuchenga mambo, mengi yamesemwa na watu tofauti, kwenye mitandao, magazeti na viongozi wake!

Hana ugomvi na kiongozi yoyote, kwa kuwa siasa sio ugomvi. Kama binadamu wa kawaida hana chuki wala hasira na binadamu mwingine yoyote!

Iwe wazi kuwa katika Taifa kuna misingi ambayo inaongoza taifa. Inapofika mahali taifa linaongozwa kwa msingi ya propaganda na upotoshwaji matokeo yake ni vurugu kubwa katika taifa. Yeye amekataa hayo yote!

Anasema kuwa YEYE hakuwa likizo kama inavyosemwa na viongozi wake! Atafafanua kwa kifupi!

Kilichotokea ni kuwa aliamua kuachana na siasa, tarehe 28 Julai 2015, majira ya saa tatu usiku, baada ya kuona yanayofanyika ndani ya chama chake hayamridhishi.

Kinachosemwa ni kuwa Dr. Slaa alishiriki tangu mwanzo kwenye mchakato. Anasema ni kweli alishirii kwenye majadiliano, akaweka msingi na msimamo wako. Kuna wakati wengi wanashinda kutokana na wingi wao, wewe unayeamini katika misingi inabidi uachie ngazi.

Baada ya Edward Lowassa kukatwa na CCM Dodoma, Mshenga wake alimpigia simu na kuuliza nini kifuate baada ya tukio la dodoma. Akamuambia wawasiliane na mwenyekiti Freeman Mbowe, Gwajima nae akafika kwenye kikao hicho.

Msimamo wa Slaa ni kuwa ni lazima kumsikiliza mtu kabla ya kuamua nini cha kufanya. chadema ni cham cha siasa na hakiwezi kumkataa mtu yeyote kujiunga na chama.

Wakaweka vijana kuchunguza nini wanataka hao wanaotaka kujiunga na chama!

Slaa akataka kwanza Lowassa atangaze kutoka kwenye chama chake alichopo, kisha atangaze anakwenda kwenye chama gani. Atumie nafasi hiyo ya mkutano huo ajisafishe na tuhuma zote ambazo amekuwa akituhumiwa na watu.

Chadema ni cham ambacho kwa muda mrefu kimejijenga kwa msingi, na ni lazima wapokee mtu ambaye hawezi kukichafua chama chao.

Lowassa hakutangaza kujitoa, wala kujisafisha hadi kwenye mkutano ambao uliandaliwa na chadema. Slaa hakuhudhuria ule mkutano.

Kwenye kila jambo kuna jambo la kuzingatia. Mtu anayejiunga popote anakuja kama mtaji au kama mzigo? Lowassa anakuja chadema kama asset au liability?

Ijulikane, suala sio urais! Mpaka siku hiyo Slaa hakuwa amechukua fomu ya Urais kwenye chama chake. Slaa hakuwa anamzuia Lowassa kugombea urais chadema. Alitaka mgombea mwenye sifa na uwezo wa kukitoa Chama cha Mapinduzi.

Hakutamka popote kuwa anataka kugombea, hata 2010 hakugombea, aliombwa kugombea! Urais wake binafsi hauwezi kuikomboa nchi bila mchango wa jamii nzima.

Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Suala la adha Lowaasa ni msizo au mtaji halikujibiwa hadi siku ya mkutano tajwa. Wakataka kujua anapokuja anakuja na akina nani, ni wafuasi wa aina gani; vijana wa bodaboda, vijana wasio na ajira au watu waliosombwa tu, au wanakuja kwenye mapambano?

Jibu lilikuwa ni kuwa tungepata wabunge 50 na wenyeviti wa CCM mkoa wasiopungua 22, wenyeviti wa CCM wilaya 88. Slaa akakiri kuwa kama ni hivyo kutakuwa na tetemeko (la kisiasa).

Wakahitaji majina ya hao waliotajwa kwa kuwa walikuwa kwenye mchakato wa kupitisha majina kwenye chama. KAtibu mkuu makini huwezi kuchukuwa watu usiowajua. Hakuna jina nililopewa mpaka tarehe 25.

Tarehe 25 wakamfata na kumuambia aitishe Kamati Kuu ya chama. Akakubali lakini akatahadjharisha kuwa hajapata majina na hajapata jibu kuwa Lowassa ni asset au liability. Lakini akaitisha kikao kwa kuwa ni jukumu la kikatiba la katiba.

Mwenyekiti akapiga simu, anasikia kuwa hajaridhika. Tangu 2004 Slaa hajawahi kugombana na mwenyekiti wake, isingekuwa sawa kama wangetofautiana kwenye kikao rasmi.

Wakakutana na Mwenyekiti, Gwajima, Lissu na wakajadiliana mpaka saa 9 mchana. Maneno kuwa alikuwa anakubaliana na mpango huo tangu mwanzo SI KWELI!

Mkutano ukashindikana. Wdau wakasema waende nyumbani kwa Lowassa, Slaa akakataa wakaenda Kamati kuu.

Kikao kikafanyika hadi saa 12 jioni. Ikaundwa kamati ndogo ya kumshawishi Slaa. Akakataa!

Akaandika barua ya kujiuzulu kwa kamati, Prof. Safari akaichana barua yake. Akaandika barua nyingine kwa Makamu-Zanzibar, makamu akamuambia kuwa haya mambo yamepangwa, asijisumbue!

Wanasema siasa ni mchezo mchafu, yeye anaaamini kuwa siasa ni sayansi! Asubuhi ya kesho akaandika barua, wasichojua ni kuwa kujiuzulu hakuhitaji barua. Maneno yakazuka kuwa Slaa hajaandika barua!

Upotoshwaji ukaendelea kuwa Slaa atazungumza na waandishi wa habari, wengine wakasema amefungiwa, amefungiwa na mkewe na kadhalika! Ukweli ni kuwa alikuwa na Lissu, Gwajima na Mbowe tangu asubuhi.

Maamuzi aliyoyafanya yanatokana nadhamiri yake!

Josephine nae ni mwanaharakati, ana sababu ya kuwa na uchungu. Alipigwa mwaka 2011 wakati wengine walijificha! Propaganda hizo tumeshazisoea!

Kama kuna mwenye ushahidi wa propaganda hizi aje, audited report zipo! Josephine halipwi na chama! Watu wanasema kuwa Slaa analipwa mil. 7, yeye ameendelea kula mihogo na maharage kama walivyoahidi mwaka 2010.

Wana uchungu na harakati!

Kikubwa katika harakati ni credibilty, jina la chama kilichojengwa kwa muda mrefu kisichafuliwe kwa namna yoyote! Mwanasiasa yoyote hataki kuchaguliwa, na Slaa nae hataki kuchaguliwa!

Wanasema kuna maslahi mapana ya taifa, ni nani anayapima? Lazima kuwe na kipimo cha kuapima hayo maslahi badala ya kutegemea mtazamo wa mtu!

Anafafanua suala la liability sasa!

Wamekuwa waongo kwa kuwa hakuna kipengele hata kimoja cha madai ya Slaa kimetekelezwa. Alisema wabunge waje kabla ya kura ya maoni ya CCM, kuja baada ya hapo ni kutafuta kichaka cha kujificha!

Watanzania wameijenga Chadema kwa damu yao, rasilimali zao! Watu hawawezi kukimbilia kirahisi wakati sio wasafi, akiwemo Sumaye na wengine. Nani hajua kama Sumaye ni fisadi? Kwa muda mrefu Slaa haongei na Sumaye kwa kuwa alimtuhumu kwa ufisaidi.

Sumaye ni mtu ambaye wanahabari walidai kuwa Sumaye alisema kuwa atahama chama endapo Lowassa atateuliwa, leo akageuka!

Leo anamsafisha Lowaasa, dhambi haisafishwa kwa dhambi. Anakumbusha jina la Mr. Zero (jina la utani la Sumaye).

Chama kimepokea makapi, na katibu alitahadharisha kuwa chama hakipokei makapi! Hakuna ambaye alijitoa kwa hiari, wengi walikuja baada ya kukatwa. Wenyeviti wengi ni mzigo, akiwemo Msindai.

Anangoja ajibu amlipue hadharani kwa kuwa alikuwa mwenyekiti wa kamati ya bunge hesabu za serikali z mitaa.

Siku aliyoambiwa aitishe kamati kuu aliuliza majina, akaambiwa anakuja chizi! Chizi ni nani, hata nyie hamumjui! Anaitwa chizi kwa kuwa ni mwizi wa kura ndani ya CCM.

Kuna haja gani ya kushindana kama tunampango wa kuiba kura pia. Wakamtaja Guninita, nani asiyemjua udhaifu wake? Hawezi kuandika hata ukurasa mmoja wa ripoti, amehama vyama mara kadhaa!

Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Viongozi wa Chadema wamepata kigugumizi, waseme nani ameongeza thamani kwenye chama?

Najua maneno ya kuwa ni lazima kuiondoa CCM kwanza hata ikibidi tuweke mkataba na shetani, mimi ni padre wa Kanisa Katoliki! Kuwaondoa CCM kwa namna yoyote hakuleti maendeleo. CCM itaondolewa kwa program siriaz, sio kutumia watu wale wale!

Lazima tujue nini kilifanya Watanzania waamini chadema, kwa kuwa waliamini wana misingi isiyoyumba na uadilifu. Leo tunasimamia uadilifu?

Wanasema mwenye ushahidi aende mahakamani. Kama tusingewatuhumu Mramba na Yona wasingefikishwa kizimbani. Chadema imefungwa mdomo kwa kisingizio cha ushahidi!

Ni bora kukaa kimya kuliko kupotosha. Anasema nukuu ya biblia kuhusu wapotoshaji!

Inapofika mahali unapoambiwa hakuna mwenye dhambi ni makosa, dhambi haisahihishwi kwa dhambi nyingine! CCM wamekuwa waoga, wamewalea watu hawa kwa muda mrefu!

Kwa Wafrika choo ni neno baya, kwa wazungu choo ni rest room! Choo cha Kitanzania huwezi kukihamisha ndani ya chumba cha kulala na ukakiita choo, huwezi kulala kwa kuwa kitanuka, tena zaidi!

Ufisadi ilikuwa ajenda iliyowapa umaarufu CHADEMA, leo wamewachukua. Waanweza kuwa na ujasiri wa kukemea ufisadi?

Mwaka 2008 Slaa alikuwa bungeni wakati wa sakata la Richmond, anafahamu kwa uzuri anachokimaanisha. Bahati mbaya waandishi hawasomi makaratasi, na wabunge wa CCM pia.

Lowassa hatuhumiwi kwa habari ya Richmond pekee!

Lowassa aliambiwa na Slaa aache kulalamika, atangaze uhalali au uharamu wa Richmond, anamtaka aseme hao 'wakubwa' ni akina nani? Ni afadhali sifa yake iharibike kuliko kusema uongo.

Ni aheri kupotea kwenye siasa za dunia kuliko kusimamia uongo!

Msingi wa kwanza wa Richmond: Ili uelewe ni lazima urudi kwenye taarifa ya Kamati ya Mwakyembe, Slaa alifuatwa asubuhi ya siku ile kupewa rushwa, anashuru Sitta na Mwakyembe wajitokeze!

Akamuuliza mtoa rushwa kama anatoa m.500 kwa mbunge, atakuwa nazo ngapi? Aliwaambia Sumaye na Lowassa kuwa rushwa ni jambo linaloanzia kifuani kwanza. Mwanzo wa jambo hili ni taarifa ya Baraza la Mawaziri la 10.2.2006. Kamati ya mwakyembe iliangalia faili la kikao kile kisha kuandika ripoti!

Suala hili lilianzia wakati wa utawala wa mkapa kutokana na dharura ya umeme nchini, wakawasiliana na kampuni moja ya Amerika Kaskazini kwa suluhu ya muda mfupi ya umeme.

Serikali ya Kikwete ikapokea lile suala. Wakaruhusu mpango uendelee, ila kwa kufuata sheria. Hiyo ilikuwa kauli ya Baraza la Mawaziri!

Wakati auala lile linaamuliwa, Lowassa alikuwa Waziri Mkuu! Na ndie mwenye mandate ya maamuzi ya Serikali, iweje leo akane kuhusika?

Taarifa ya Mwakyembe inapotoshwa! Taarifa ilitaka Waziri Mkuu ajipime, au bunge limjadili na kumchukulia hatua. Lowassa akakimbia kwa kuwa alijua Bunge lingemfukuza kazi!

Waliioomba tenda walikuwa 26, waliorudisha walikuwa 8. Kamati ya Tathmini ikaona hakuna anayefaa hata mmoja! Waziri Msabaha akaagiza taarifa ile ifutwe na tathmini ifanyike upya, mara ya kwanza, ya pili, ya tatu na ya nne. Jeuri wa Msabaha ilitoka wapi?

Baraza likaamua baadaye tenda iliyopewa kwa kampuni ya kwanza ifutwe! Lowassa alishiriki!

TANESCO wakatoa ushauriwa wao, Mamlaka husika ikatafute internatonal tender ya kununua turbine!

Lowassa akaingilia mchakato dakika za mwisho, akamuagiza katibu muhtasi wake!

Kwanini Lowassa, kwa kuwa anagombea urais, rais asiyeaminika hawezi kuchaguliwa!

Lowassa alishawahi kumuita Slaa kuhusu habari ya Meremeta, na kumuambia kuwa taarifa yake inaiaibisha Serikali! Kampuni ya jeshi imewahi kutengeneza gari, imehujumiwa na wahuni. Akamtaka Lowassa amuambie ni nani aliyehusika?

Akamuita mwingine kwnye Speaker lounge. Slaa akamuambia kuwa yeye ni fisadi kichwani, rohoni mpaka...!

Tunamsifia Lowassa kuwa an=taleta maji wakti jimbo la Lowassa halina maji na ufisadi mkubwa umefanyika kwneye jimbo hilo. Mnazungumzia shule za kata wakati wakati hamjua zimeanza wapi?

Slaa anataja nafasi alizowahi kushika Afrika. Uamuzi wa kujenga shule za kata ulifikiwa mwaka 90 huko Thailand, mpango huo ukaitwa Education for All, sio MMES kama unavyoitwa leo!

Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Anasoma barua ya Ibrahim Msabaha kwa Flugence Kazaura, mkurugenzi wa bodi wa TANESCO!

Mpango ulikuwa kuondoa suala la umeme mikononi mwa tanesko kwa kuwa imeshindwa kutekeleza. Ugomvi wake na Masha ni kwa kuwa Lowassa alimlaumu Masha kuingilia mchakato wa serikali, akawekewa kinasa sauti chumbani.

Waziri Mkuu haruhusiwi na sheria kuingilia mchakato wowote wa tenda.

Kwenye kampuni nane zilizowasilisha maombi ya zabuni, Richmond ni kampuni iliyokuwa mbovu. Ilikuwa ni kampuni ya steshenari, sio umeme!Wakadai wana ushirikiano na kampuni nyingine ya umeme, kampuni hiyo ikakataa kujihusisha na Richmond, wala kuzalisha na majenereta!

Bill Clinton aliwai kukutwa na kashfa, walitaka kumchukulia hatua si kwa sababu ya zinaa, bali kwa kuwa alifanya uongo! Kwa kuwa alidanganya umma! Hata sheria za Tanzania zinakataza kuongopa, hata kesi za uchaguzi za Slaa zimethibitisha hilo.

Lowassa anadai yeye alisimamisha tenda, Slaa anaonesha uthibitisho wa hilo kwa barua za Lowassa kwenda kwa Msabaha zinazokanusha hilo, 'Anaisoma'! Waziri Mkuu aliharakisha mchakato wa tenda, tofauti na sheria ya PPRA. Barua imeandikwa miezi mitatu baada ya mkataba kusainiwa, kwa maagizo ya Waziri Mkuu.

Tanesko ikaagizwa kusaini mkataba ambao haikuhusika kwenye kuujadili! Anaona aishie hapo... Anaupigia chapuo mdahalo wa Sitta na Mwakyembe, anasema Lowaasa nae afike kuondoa utata na kusema ukweli!

Chadema ni chama kilichotoa matumaini kwa vijana wengi! Isifike mahali tukawa washabiki kama 2005 ambapo watu waliahidiwa maisha bora, wakajikaanga kutokana na ushabiki! Anatoa ushahidi wa kitakwimu wa mfumuko wa bei...

Slaa ana uchungu kuona chama alichokijenga, kikifikia hatua ya kusomba watu kwa mabasi na malori kisha mkasema mafuriko hayazuiliki! Hayuko tayari,... Anakataa kuwa ZEZETA!

Ajenda ya Chadema ni nini, ilikuwa ni rushwa! Wananchi waliamini kwa kuwa msingi huo ndio unakijenga chama!

Sehemu kubwa ya kilichosemwa Jangwani ni ilani ambayo ilishaandaliwa tayri, hakuna kipya kilichosemwa. Kinachomuuma ni chama makini kuwa kibovu zaidi ya Chama cha Mapinduzi!

Hatuwezi kujenga maadili tukiwa na watu wachafu, anaishi na mwanamke bila kufunga ndoa kwa kuwa Serikali ya CCM haitaki afunge ndoa. Kesi yake ililetwa na mawaziri, waandishi wa habari na mtu kutoka IKULU. Ndoa inafungwa na Mungu!

Scotland Yard iliamrisha Lowassa achunguzwe, inakuwaje leo tunamtetea? Huu ni ushabiki usio na vielelezo, Slaa ana ushahidi! Hakuna ulazima wa kwenda mahakamani kwa kuwa kesi ya rushwa ni jinai, ni kesi ya serikali! Slaa au mwingine hana locus ya kwenda mahakamani kwa kesi ya jinai!

Mwakyembe alisema kesi ya jinai haina mwisho (kama zilizyo za madai).

chadema iliahidi kusafisha nchi kwanza endapo itashika dola, huku maendeleo yakiendelea!

Anasoma barua ya mchakato wa Richmond kuwa DOWANS. Kampuni imesajiliwa Costa Rica, na mwenyekiti asiye na anuani, simu wala jengo! Siku iliyosajiliwa, mmiliki alisajili makampuni mengine 99! Zaidi ya hayo ana makampuni mengine zaidi ya 50, DOWANS ni jina tu. Kampuni haipo!

Dowans sio kampuni halisi huko Kosta Rika, nchi nzima hakuna kampuni yenye uwezo wa kuzalisha umeme kwa kiwango hicho!

Leo Lowaassa anatuambia tufunge mdomo, huu ni udikteta! Anakumbusha sakata lake na Waziri Marmo...

Mabilioni ya fedha yanalipwa kwa kampuni ambayo haipo! Tunapenda ushabiki... Acha sifa iharibike!

Anasema hataki kuingia kwenye mambo ya Babu Seya! Vyuo vikuu vinatumia kesi ya Babu Seya kama case study. Mtoto mdogo hawezi kutoa ushahidi mahakamani, haki inapuuzwa kwa kuwa mtoto hawezi kutoa ushahidi!

Kesi ya Ulawiti rais hana mamlaka nayo, anatoa wapi kiburi cha kusema kuwa atamtoa?

Aliyeagiza polisi kuingia na polisi kuingia na mbwa msikiti wa mwembechai ni Sumaye, akiwa waziri mkubwa. Leo hii ni mpiga kampeni wa Lowassa! Leo tunataka kura kwa namna yoyote!

Ni afadhali kutokuwa na rais wa aina ya mtu huyu! anayesaka kura kwa kusaka huruma za watu. Slaa hayuko tayari kuona hilo linatokea...

Anahitimisha kwa kusema hajagusa chochote kuhusu ilani wala mkakati!

Mwafrika, [01.09.15 15:45]
Kama taifa tuna kazi kubwa ya kuchambua vitu nje ya shamrashamra, maneno matamu! Tumeshaumwa na nyoka, tusilaghaiwe na maneno ya watu hawa tena!

Utendaji uliotukuka unapimwa kwa utafiti, sio kwa ukasuku na kunukuu maneno ya wanasiasa!

Lowassa alipokuwa Waziri Mkuu, matatizo ya wakulima na wafugaji yalikuwepo, alifanya nini? Lowassa aliwahi kubadili mpaka wa Monduli na Karatu na kusababisha mgogoro!

Mkampenia wake, Sumaye alisababisha matatizo ya ardhi Mvomero, akipora ardhi ambayo ilitakiwa yajengwe makao makuu ya Mvomero! Mengine ya Sumaye ameyaweka kiporo, hisa zake za kampuni aziweke wazi kama Sekretarieti ya Maadili inavyotaka!

Kutotangaza mali kunatosha kumtoa mtu ubunge! Sembuse Urais?

============================== =========================

Ukweli huwa una tabia ya kuegemea upande, anasemea speculation kuwa ameisema chadema peke yake.

Anasema amestaafu siasa, hana chama lakini bado anabaki kuwa mtanzania, mtetezi wa wanyonge na atabaki hivyo! Ataendelea kuwatumikia watanzania kadiri ya Mungu alivyomjalia vipawa! Kama alivyoombwa kugombea urais 2010!

Anaweza kuwatumikia Watanzania bila kuwa na chama!

Anasema kuwa hajapata vitisho kama alivyopata kipindi hiki, inazidi hata wakati alipotangaza List of Shame. Rostam ndiye anafadhili kampeni za urais wa Lowassa! Anamnukuu vitisho vyake! anakiri kuwa maaskofu wamehongwa, Rostam akiwa anaona, m60-m300!

Anasema hatenda chama chochote, anasisitiza! Amejitoa rasmi siasa za vyama vya siasa... Ataendelea kuwa msimamiaji wa anachokiamini!

Anawataka watu aliowataja watoke hadharani, anatoa baraka za KIMUNGU kwa nchi na watu wake!
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top