Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

LOWASSA AIFUTA CCM JIMBO LA MONDULI, AMTAJA MRITHI WAKE

Mh. Lowassa akihutubia mkutano huo wa kampeni



Mgombea jubunge jimbo la Arumeru Mashariki, Mh. Joshua Nassary, akizikusanya kadi za Wanachama wa CCM zilizorudishwa na kujiunga na Chadema, wakati wa Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Polisi, Monduli Mjini leo Oktoba 5, 2015

Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Monduli kwa tiketi ya CHADEMA, Julius Kalanga, wakati wa Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Polisi, Monduli Mjini leo Oktoba 5, 2015

Wananchi wa Monduli wakimpokea kwa shangwe, mpendwa wao ambaye ni Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, wakati akiwasili kwenye Uwanja wa Polisi, Monduli Mjini, leo Oktoba 5, 2015

Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa na Mkewe Mama Regina Lowassa, wakishiriki tendo la kimila ya Jamii ya Watu wa Kimasaai lililoongozwa na Malaigwanani, wakati akiwasili kwenye Uwanja wa Polisi, Monduli Mjini, leo Oktoba 5, 2015
 Picha ya juu na chini, Mh. Lowassa akihutubia mkutano huo wa kampeni

 
Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), anayewakilisha vuguvugu la UKAWA, Mh. Edward Lowassa na Waziri Mkuu wa Zamani, Mh. Fredrick Sumaye, wakionyesha lundo la kadi za wanachama wa CCM wa Wilaya ya Monduli, waliozirudisha ili kuungana na Watanzania wote kwenye harakati ya Mabadiliko, wakati wa  Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Polisi, Monduli Mjini leo Oktoba 5, 2015. Kulia ni Aliekuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Monduli, Rubein Ole Kuney aliejiunga na Chadema.Picha na Othman Michuzi, Monduli. (Picha na Othman Michuzi)
NA K-VIS MEDIA
ULE msemo wa Kiswahili usemao “mcheza kwao hutunzwa” umedhihirika leo wilayani Monduli, baada ya mgombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CHADEMA, akiwakilisha vyama vine vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA, Mh. Edward Lowassa, ametua jimboni kwake “nyumbani” Monduli, na kuhutubia mkutano mkubwa wa kampeni ambapo wanachama kadhaa wa CCM, wamerudisha kadi na kujiunga na UKAWA.

Wanachama hao wa CCM waliokihama chama hicho, waliongozwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Monduli, Reuben Ole Kuney.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top