Waendesha pikipiki maarufu kwa
jina la bodaboda na bajaji zaidi ya mianne wamefunga barabara kuu
itokayo Dodoma hadi Mwanza kwa zaidi ya saa moja, kwa madai kuwa mwenzao
ambaye ana hali mbaya baada ya kupigwa na kitu kizito kichwani na
askari wa jeshi la polisi baada ya kugongana.
Wakitoa malalamiko yao na baadaye
kufanya maandamano hadi ofisi ya mkuu wa jeshi la polisi wamesema baada
ya mwenzao kupigwa hakuna hatua zozote zimechukuliwa na jeshi hilo.
Baada ya maandamano kuanza na kufunga barabara hali ilikuwa hivi.
Kutokana na usumbufu wa kuzuia
magari na kuwazuwia baadhi yao ambao walikuwa wakifanya biashara ya
kupeleka abiria jeshi la polisi baada ya kuwaomba kufungua barabara na
kukaidi amri hiyo liliamua kutumina nguvu kwa kupiga mabomu ya machozi
na kufanikiwa kuwatawanya huku wengine wakishikiliwa.
Kwa upande wake daktari wa mkoa
wa Singida, Daktari Geofry Mgeta amesema kuwa hakuna mgonjwa aliye
fikishwa hospitalini akiwa majeruhi kwa kupigwa na chuma la kufungulia
matairi na kupatiwa rufaa ya matibabu nje ya mkoa isipokuwa wana
wagonjwa madereva wawili wa bodaboda walio pigwa na kutaka kuchinjwa
wakati wakitaka kuporwa pikipiki zao.
Akiongea kwa njia ya simu kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida Thobiasi Sedoyeka amekiri kuwepo kwa tukio hilo na kusema kuwa askari wa jeshi la polisi aliyegongana na pikipiki, wakati wanafanya utaratibu wa kisheria ndipo vurugu zilipoanza na madereva wa bodaboda walitaka kuchoma moto gari lake nayeye kuamua kujilinda kwa kuchukuwa spana ya kufungulia tairi na kumpiganayo dereva wa bodaboda.
Post a Comment