Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ALI KIBA KUSHUSHA BALAA LINGINE

Msanii Ali Kiba ambaye kwa sasa anafanya poa na kazi yake ya Lupela amefunguka na kusema kuwa muda si mrefu kutoka sasa ataachia kazi nyingine mpya.

Akipiga stori kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, Ali Kiba amedai kuwa kazi yake hiyo anayotaka kuiachia mpaka sasa hana jina lake lakini atawaachia mashabiki ambao ndiyo watakuwa na jina la kazi hiyo.

"Mashabiki zangu kaeni mkao wa kula nashusha balaa lingine muda si mrefu kutoka sasa. Hii ngoma hata sijui mimi niiiteje yaani ila nitawaachia wenyewe wananchi mchague jina la kazi hiyo" alisema Ali Kiba.

Mbali na hilo Ali Kiba amesema kuwa kitendo chake cha kutoa wimbo bila video kimekuwa na athari kubwa kwake kwani wimbo unakuwa mkubwa na mashabiki wanakuwa tayari na video zao vichwani mwao, kiasi kwamba anapokuja kutoa video ya wimbo huo unakuwa tofauti na mategemeo na matarajio ya baadhi ya watu jambo ambalo huwa linaleta maneno maneno.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top