Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ZITO KABWE ATOA MCHANGANUO RASMI WA BAJETI YA 2016/2017

 Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya Chama cha ACT Wazalendo ametoa mchanganuo wa bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2016/17, ambayo wabunge wote walikuwa wanaijadili siku ya leo.

Katika ukurasa wake wa facebook Mh. Zitto kabwe ametoa mchanganuo huo wenye vyanzo vya upatikanaji wa fedha hizo, huku akisema kiasi kamili cha bajeti hiyo ni kizuri na chenye kuleta matumaini.

“Bajeti ya mwaka 2016/17 ni tshs 29.5 trillions,TRA watakusanya tshs 17.8 trilioni, mikopo itachukuliwa tshs 7.5 trilioni na misaada ya wafadhili 3.6 trilioni, matumizi ya kawaida tshs 17 trilioni na Matumizi ya Maendeleo 11.8 trilioni. Bajeti ya tshs 29.5 trilioni ni hatua kubwa sana”, aliandika Mh. Zitto Kabwe.

Pia Mh. Zitto ameweka wazi kuwa serikali ina mpango wa kukopa kiasi cha shilingi trilioni 2.1, kutoka nje ya nchi, mkopo ambao utakuwa na masharti ya kibiashara.

Pamoja na hayo Zitto Kabwe amesema kitendo cha serikali kutaka kurasimisha sekta zisizo rasmi itasaidia kukuza pato la taifa, kwani itawezesha hata wafanyabiashara wadogo kulipa kodi.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top