Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CHAMA CHA WAFANYAKAZI WA BUNGE CHAPATA MWENYEKITI MPYA

Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Mkoa wa Dodoma Bw. Mchenya John akizungumza na wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge (hawapo pichani) kabla ya Uchaguzi wa Viongozi wa TUGHE tawi la Bunge uliofanyika mapema wiki hii Mkoani Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Ofisi hiyo Bibi. Emma Lyimo.Mwenyekiti aliyemaliza muda wake kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) tawi la Bunge Bw. Abdallah Hancha (wa kwanza kulia) akitoa neno la shukrani kwa wafanyakazi wenzie wa Ofisi ya Bunge kabla ya kuanza kwa uchaguzi wa TUGHE uliofanyika mapema wiki hii Mkoani Dodoma. Walioambatana naye ni wajumbe wa Kamati Kuu ya TUGHE tawi la Bunge.Wasaidizi wa kamati ya Uchaguzi wakihesabu kura wakati wa Uchaguzi wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) tawi la Bunge uliofanyika mapema wiki hii kwenye Ofisi za Bunge Mkoani Dodoma.Mwenyekiti mpya wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) tawi la Bunge Bw. Chacha Nyakega akizungumza mara baada ya kutangazwa mshindi wa uchaguzi wa TUGHE uliofanyika mapema wiki hii kwenye Ofisi za Bunge Mkoani Dodoma.

PICHA ZOTE NA FATMA SALUM-MAELEZO
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top