Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

IFM WAELEZEA UFISADI WA MAMILIONI CHUONI HAPO




Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kimesikitishwa na habari zilizochapishwa na gazeti la RAI Toleo la 1249 la tarehe 5 – 11 Mei 2016 ambazo ni za upotoshaji.

Tunapenda kufafanua kuwa taarifa za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) zinaeleza kuwa, Chuo cha Usimamizi wa Fedha kilipokea fedha za ziada kutoka Wizara ya Fedha kwa ajili ya mishahara na fedha hizo zilishapangwa kurudishwa ndani ya mwaka wa fedha 2015/2016 kama ripoti ya Mkaguzi ilivyoagiza katika mwaka wa fedha wa 2014/2015.  Kwa hiyo fedha hizo hazijatafunwa wala kupotea.

Kuhusu ukusanyaji wa madeni yaliyoripotiwa, nusu ya deni ni karo ya wanafunzi wanaolipiwa na Bodi ya Mikopo na fedha hiyo ililipwa Chuoni ndani ya mwaka wa fedha 2014/2015.  

Madeni mengine ni ya wanafunzi walioshindwa kuendelea na masomo kwa sababu mbalimbali na madeni hayo yanafutwa kwa kufuata taratibu za kifedha (Financial Regulation) kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali alivyoelekeza.

Ufanunuzi huu ulitolewa kwa mwandishi wa gazeti hili (Bwana Gabriel Mushi) mnamo tarehe 04-05-2016 alipoongea na Naibu Mkuu wa Chuo Mipango, Fedha na Utawala.

Kwa kumalizia Chuo cha Usimamizi wa Fedha kinafanya kazi zake kwa kufuata taratibu zilizowekwa na kwa zaidi ya miaka 30 mfululizo Chuo kimepata hati safi za mahesabu (Clean Audit Report) kwa mujibu wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG).
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top