Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAAJABU .... MAMA AJIFUNGUA MAPACHA WATANO

160510092135_tucci_quints1
160510092135_tucci_quints1
Mama mmoja raia wa Australia ametoa picha za mapacha watano aliowazaa mwezi Januari.
Watoto Keith, Ali, Penelope, Tiffany na Beatrix

Kim Tucci wa miaka 26 alichukua dadika mbili tu kujifungua wanawe hao, wasichana wanne na mvulana mmoja.
160510092135_tucci_quints2
Wote walitungwa kawaida, hakutumia matibabu yeyote ya uzazi.
160510092135_tucci_quints2
Familia inasema watoto huvishwa vibinda 350 kwa wiki

Madaktari 50 walimsaidia mama huyo kujifungua kwa njiya ya upasuaji, na wanawe wote wako shwari.Wanasayansi wanasema ni mama mmoja kati ya milioni 55 ana nafasi ya kuzaa mapacha watano.
Bi Tucci alipata umaarufu sana wakati alipoweka taarifa za mimba yake katika ukurasa wake wa Facebook.Kampuni ya kunasa picha ya Erin Elizabeth imesaidia sana kunadi safari ya Bi Tucci wakati wa uja uzito wake.
160510092136_tucci_quints3
160510092136_tucci_quints3
Kim Tucci akiwa mja mzito na pacha wake

Mama huyo ameelezea changamoto alizokumbana nazo akisema kwa wakati mmoja alihisi kama anapoteza maisha.Ameongeza madaktari walimshauri kuwaokoa watoto wawili na kumtaka kuwatoa wengine kutokana na sababu za kiafya.
Hata hivyo aliamua kubeba mimba yake hadi mwisho.
Bi Tucci na mumewe bwana Vaughn wana watoto watatu mvulana na wasichana wawili.Wameanza kuchangisha pesa ili kununua gari kubwa ambalo litaweza kukimu familia hiyo kubwa.
Source: BBC
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top