Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MADIWANI WA MISUNGWI WACHARUKA, NI BAADA YA MBUNGE WAO KITWANGA KUTUMBULIWA ... WATAKA BUNGE LIOMBE RADHI

UTANGULIZI
Rais Dk. John Pombe Magufuli kutengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga.

Tunaamini kwa uwezo mliona kama waandishi wa habari, taarifa hii itafikia umma wa Watanzania kama ilivyokusudiwa.

UFAFANUZI
Kama mnakumbuka mnamo tarehe 20 Mei mwaka huu, Rais Dk John Pombe Magufuli alichukuwa uamuzi wa kutengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga ambaye pia ni Mbunge wa Misungwi kwa kosa la kwamba Mhe. Kitwanga aliingia bungeni akiwa amelewa.

Sisi wananchi wa Jimbo la Misungwi tumesikitishwa sana na taarifa na uamuzi huu kwa kuwa tunaamini kuwa kuna dhamira iliyojifika iliyopelekea Mhe Rais kufanya maamuzi haya. 

Ukweli ni kwamba huu ulikuwa mpango wenye dhamira ovu na uliogubikwa na uongo mwingi ukilenga kumchonganisha Mbunge wetu na Mhe. Raisi uliopangwa na waovu wachache ambao wamebanwa na Serikali hii ya Awamu ya tano kupitia wizara hiyo nyeti kwa usalama wa nchi.
Itakumbukwa kuwa, Mhe Charles kitwanga alinadiwa na Mhe Rais na wanaCCM na baadae kupigiwa kura kwa wingi na wananchi wa Misungwi kwa ajili ya uwezo wake na dhamira yake njema ya kulinda taifa letu. 

Sisi wananchi wake, tunaamini katika uwexo wake, uadilifu wake na nidhamu ya kazi aliyonayo, hatuna mashaka na hili.

Baada ya kuteuliwa na Mhe Raisi kama Waziri wa mambo ya ndani, amekuwa muadilifu na kafanya mengi katika kuimarisha usalama na kufanya maamuzi yengi mazuri kwa maslahi ya taifa. 

Hili lilimtengenezea maadui wengi ndani ya serikali, ndani na nje ya CCM, mtandao wa dawa za kulevya, walioachishwa kazi NIDA na Uhamiaji. 

Watu hawa ndio waliochochea na kutengeneza mkakati wa kumchafua Mhe Kitwanga na walikuja dodoma kuhakikisha dhamira yao ovu inatimia.

USHAHIDI WETU
Miongoni mwetu tulikuwa mjini Dodoma pamoja na madiwani wa Jimbo la Misungwi ambao tulikwenda kumtembelea Mbunge wetu bungeni, tulizungumza mengi kwa ajili ya jimbo letu na katika kikao chetu hapakuwa na chembe ya kilevi chochote na hata kesho yake alipoinga bungeni alikuwa mzima wa afya ya kimwili na akili timamu na tunawahakikishieni kuwa Kitwanga hakuwa amelewa.

Ndugu waandishi wa habari asubuhi ya tarehe 20 tulielekea bungeni kwa mwaliko wa Charles Kitwanga, tukiwa sehemu ya mualiko uliowajumuisha Madiwani wa jimbo lake tukiwa tumeambatana naye tukaingia ndani ya ukumbi wa bunge,tukashuhudia anajibu swali,baada ya kujibu swali la mbunge Sakaya,tulitoka nje na kupiga picha na madiwani wote wa Misungwi waliokuja kumtembelea Dodoma.

Baada ya zoezi la kupiga picha kukamilika pale nje ya ukumbi wa Bunge, tulitoka na kuelekea Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwa lengo la kututembeza maeneo yote ya Dodoma , lakini ilipofika jioni wakati tukirejea nyumbani tukiwa naye, ghafla tukaona habari zikisambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Waziri Kitwanga amevuliwa uongozi kwa kuwa alionekana na Waziri Mkuu akiwa amelewa.

Ndugu wanahabari , tulishangazwa wote kwani tulikuwa tumekaa naye pale nyumbani kwake Dodoma (site 2) tukipata chakula cha usiku ,alionekana kutoaamini na hata madiwani pia na wengine ambao tulikuwepo hapa nyumbani kwake hatukuamini.

Tunachosema ni kwamba waziri Kitwanga hakulewa kama ambavyo imepotoshwa, bali ulikuwa ni mkakati wa kumchafua na kuhakikisha anavuliwa wadhifa wake ili watu hawa waendelee kufanya maovu yao. 

Mtandao wa dawa za kulevya, pamoja na wale waliokuwa wanamshutumu kwamba amehusika kuondolewa kwao kazini wakiwemo Watu wa NIDA, Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete, Mfanyabiashara Said Lugumi pamoja na kundi mafisadi waliokwapua mabilioni ya fedha NSSF. 

Pia na baadhi ya wabunge wa CCM na Upinzani ambao walikuwa hawafurahishwi na kasi ya utendaji kazi wa Kitwanga katika Wizara ya Mambo ya ndani.

Kwa niaba ya wananchi wenzetu tunamuomba na kumtahadharisha Mhe. Rais awe makini na makundi la wafanyabiashara wa madawa ya kulevya, pamoja na lile kundi la wanamtandao masalia ndani ya CCM na serikalini na kwenye vyombo nyeti vya ulinzi na usalama, ambayo kwa ujumla yalikuwa na mkakati kabambe wa kuhakikisha wanamtenganisha na kumpotosha Mhe Raisin a kumjaza habari zisizo za kweli.

Ndugu waandishi wa habari, kilichotushangaza zaidi baada tu ya Kitwanga kuvuliwa madaraka yake ya uwaziri, kuna watu walianza kufanya sherehe wakishangilia hususani wale waliovuliwa madaraka NIDA pamoja na NSSF,Uhamiaji na wale wanaotuhumiwa kuhusika na madawa ya kulevya.

Ndugu waandishi wa habari, tunajua namna kundi la Said Lugumi, Ridhiwani Kikwete na kampuni yao walivyokuwa wanadhamini kwa mbinu za kifedha katika vita hii ya kitwanga ili aondolewe, lakini baada ya kuondolewa, wakajifanya kutoa taarifa ya kushangazwa kuondolewa kwake,

Kitwanga amekuwa mtumishi wa serikali akiwa mtumishi mwandamizi benki kuu Tanzania (BOT),amekuwa mbunge na Naibu waziri kwa miaka 10,lakini hata siku moja hakuwahi kuonekana amelewa. Ni muadilifu na ana nidhamu ya kazi, na nidhamu hii ndiyo iliyomfanya aaminiwe na kupewa dhamana hii.

MAAZIMIO YETU
=Tunaliomba Bunge kumuomba radhi Mhe. Charles Kitwanga kwa kumdharirisha mbele ya wapiga kura wake wa Jimbo la Misungwi familia yake pamoja na watanzania wote waliokuwa wanaamini utendaji wake kupitia video iliyochezewa na wataalamu wa IT katika studio za Bunge ili kufanikisha lengo la kumuonyesha Kitwanga kuwa alikuwa amelewa bungeni.

=Tunamuomba Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye ndiye Kiongozi Mkuu wa Serikali bungeni atoe uthibitisho wa kikemia unaotanabaisha wazi kama Kitwanga alikuwa katumia kilevi wakati akiwa bungeni maana hakuna kipimo chochote kilichofanyika kudhibitisha uvumi huu.

=Tunaliomba Bunge lifanye uchunguzi na kubaini wale wote waliosambaza ile video inayoonyesha Kitwanga akiwa anaongea na kuonekana amelewa wakati kiuhalisia hakulewa na alijibu maswali yote vizuri

=Tunaliomba Bunge kuchunguza idara ya habari ya Bunge pamoja na studio ile ya Bunge ambao wamehusika na kuhariri ile picha ya video iliyokuwa inasambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

=Tunahoji uhalali wa kumvua mtu madaraka kwa sababu ya ulevi bila uthibitisho wa daktari ambaye kisheria ndiye mwenye mamlaka hayo kugundua kilevi cha mtu.

= Tunaomba Watanzania wote waliosikitishwa na taarifa hizi wajue tu kwamba ile video ambayo imemtia hatiani Kitwanga ilihaririwa kwa ustadi mkubwa kupitia wafanyakazi wa Bunge ambao wanapitia zile asadi za bunge pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa serikali kwenye vyombo vya ulinzi na usalama ambao hawakupenda kitwanga aendelee kuwa pale ,kwa nia ya kumhujumu na sasa wanasema kwenye vyombo vya habari ili kuhalalisha uhujumu huo.

=Tunaomba mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) kuangalia picha zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii dhidi ya Mhe Mbunge wa Misungwi ambazo zinaonekana kumchafua wachukue hatua dhidi ya watu hao kwani kisiasa zinaendelea kumchafua na kumharibia kwa wapigakura wake,familia yake,mama yake mzazi ,ndugu zake .

=Tunajiandaa kuchukua hatua kwa Bunge za kisheria kama watashindwa kuthibitisha tuhuma hizo dhidi ya Charles Kitwanga ambazo tunaamini zimetengenezwa kwa maslahi ya makundi yanayompinga ndani ya Serikali wakiwemo mtandao wa dawa za kulevya.

Pia tunamuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa makini kundi la wanamtandao walio ndani ya serikali ambalo linaongozwa wahafidhina wasio taka mabadiliko ndani ya serikali .

Imeandaliwa na madiwani wa Jimbo la Misungwi pamoja na wakereketwa wa jimbo hilo.Baraka Kingamkono,Gaudency Tungaraza na IDDY Majumuisho.

Asanteni na Mungu awabariki
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top