Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAKAMU WA RAIS ASAFIRI TENA NJE YA NCHI

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan anaondoka nchini leo kwenda Papua New Guinea ambako atamwakilisha Rais John Magufuli katika mkutano wa Wakuu wa nchi za Afrika, Caribbean na Pacific (ACP) ambao utafanyika kuanzia Mei 30 hadi Juni 01, mwaka huu.

Mkutano wa Papua New Guinea ambao utatanguliwa na mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za ACP utafanyika chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu wa nchi hiyo Mhe. Peter O'Neil.Kauli mbiu ya mkutano huo wa mwaka huu ni "Umuhimu wa nchi za ACP kujipanga kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za maendeleo endelevu."

Maeneo ya mjadala ni pamoja na kukuza usawa na maendeleo endelevu kwa ajili ya wananchi wa nchi wanachama, kuimarisha majukumu ya nchi za ACP katika utawala bora na maendeleo na pia masuala ya amani, usalama and utulivu wa kisiasa kama ni sharti mojawapo kwa maendeleo.
Kwa sasa umoja huo wa ACP una nchi wanachama 79 ambapo kati ya hizo nchi 48 ni za kutoka kusini mwa jangwa la Sahara, 16 kutoka Caribbean na 15 kutoka Pacific.

Umoja wa nchi za ACP ulianzishwa baada ya kusainiwa kwa Mkataba wa Georgetown mwaka 1975 kwa msaada wa iliyokuwa Tume ya Uchumi ya Ulaya kwa madhumuni ya kuratibu ushirikiano baina ya nchi wanachama na Umoja wa Ulaya ukizingatia kwamba nyingi ya nchi hizo ni makoloni ya nchi za ulaya.

Katika msafara huo Makamu wa Rais amefuatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dk. Servacius Likwelile na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Balozi Celestine Mushi.
Makamu wa Rais na ujumbe wake anatarajia kurudi nchini Juni 3,mwaka huu.

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
Dar es salaam
27/5/2016
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top