Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAREKANI YATOA SALUTI KWA WAPIGANAJI WA TANZANIA

Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Marekani linaloshughulikia masuala ya kijeshi barani Afrika, Meja Jenerali Darrly Williams, amemtunuku mkuu wa majeshi ya vikosi vya nchi kavu Tanzania Meja Jenerali James Mwakibolwa nishani ya ulipuaji bora wa mizinga nchini.

Nishani hiyo ambayo imekuwa ikitolewa na Rais wa Marekani, alitunukiwa Meja Jenerali Mwakibolwa baada ya kuwa mstari wa mbele kurudisha amani kwenye nchi zinazokabiliwa na vita barani Afrika.

Akizungumza wakati wa kufunga mkutano wa wakuu makamandi wa vikosi vya nchi kavu barani Afrika, uliofanyika mkoani Arusha, Jenerali Williams alisema jeshi la Marekani barani Afrika, linamtambua Mwakibolwa kuwa mchapa kazi bora. 

“Mwakibolwa ni mtaalamu sana kwenye masuala ya mizinga, hata tulipokwenda kwenye mafunzo ya kijeshi katika kambi ya Monduli, tumeona umahiri wake na tuzo hii anastahili kwa kuwa anafanya vizuri.

 “Jeshi la Tanzania limekuwa mstari wa mbele kutoa kikundi cha M23 kwenye nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na yote hayo ni kutokana na uchapakazi wa Jenerali Mwakibolwa,” alisema Jenerali Williams.

Akitoa maoni yake kuhusu tuzo hiyo, Jenerali Mwakibolwa aliahidi kuhakikisha Jeshi la Tanzania linakuwa imara zadi barani Afrika.

Alisema Tanzania inazingatia masuala ya kijinsia katika jeshi hilo na sasa asilimia 25 ya wanajeshi ni wanawake.

“Jeshi la Tanzania tuna wanawake wenye vyeo vikubwa na wako ambao tumewapa kazi kwenye idara mbalimbali. Tunaamini mwanamke anaweza,” alisema Jenerali Mwakibolwa.

Kuhusu maazimio ya mkutano huo, alisema wanaangalia namna ya kutoa mafunzo ya kupambana na ugaidi wa baadhi ya wanajeshi wa Afrika.

Naibu Katibu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Tanzania, Immaculate Ngwale alisema mkutano huo umekuwa na faida kwa kuwajengea uimara askari wake.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top