Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA POLE KUFUATIA MAUAJI YA WATU WATATU MSIKITINI MWANZA


Rais John Magufuli ametoa salamu za pole kwa wakazi wa mkoa wa Mwanza, kutokana na mauaji ya watu watatu, waliouawa kwa kukatwa mapanga wakiwa msikitini.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, jijini Dar es Salaam jana, ilisema Rais Magufuli amesema yupo pamoja na wakazi wa mkoa huo wa Mwanza katika kipindi hiki cha majonzi, kuomboleza watu hao na pia alisema anawaombea wale waliojeruhiwa wapone.

Wakati huo huo, Wizara ya Mambo ya Ndani imesema imesikitishwa na mauaji ya watu hao watatu, waliouawa msikitini katika wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.

Kauli hiyo ya Serikali, ilitolewa bungeni mjini Dodoma jana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Masauni Yussuf Masauni.

Masauni alisema kuwa Serikali inawapa pole wakazi wa Mwanza, viongozi wa mkoa na wilaya ya Nyamagana na mbunge wa jimbo hilo, Stanslaus Mabula.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top