Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SAKATAVLA LUGUMI BADO LAITESA SERIKALI


SAKATA la Kampuni ya Lugumi limesababisha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuagiza kupitiwa upya mikataba yote.
 
Kauli hiyo imetolewa leo na Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakati akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wakuu na waandamizi wa vyombo vya usalama vilivyopo chini ya wizara hiyo.

Kampuni ya Lugumi iliyoingia mkataba wa Sh 37 bilioni na Jeshi la Polisi kwa ajili ya kufunga mashine za kielektroniki za kuchukua alama za vidole nchi nzima, haikutimiza matakwa ya mkataba wake baada ya kufunga mashine 14 tu kati ya 108 ilizotakiwa kufunga licha ya kulipwa  asilimia 99 ya fedha kwa mujibu wa mkataba.

Masauni amesema, kutokana na kuwepo kwa utata wa mikataba, wizara imeagiza mikataba yote kupitiwa upya na ile ambayo itabainika kuwa na kasoro, itavunjwa.

“Mikataba yote ambayo majeshi haya yameingia ihakikiwe na ipitiwe upya ili iweze kurekebishwa na kazi hiyo iende haraka sana ili kuleta tija kwa wananchi wetu,” amesema Masauni.

Mbali na hilo ameiagiza Idara ya Uhamiaji nchini kuhakikisha inawachukulia hatua kali wale wote ambao wanaonekana kufanya kazi kinyume na misingi ya jeshi hilo.

“Kuanzia kesho naagiza kuhakikisha wanachukuliwa hatua wale wote ambao hawaendani na kasi yetu ya utendaji wa kazi na kuwaleta vijana vijana ambao wanaendana na kasi yetu ya hapa ni kazi tu.

“Kumekuwepo na shida kubwa katika maofisa wetu wa Idara ya Uhamiaji wanaohusika na mambo ya uchunguzi ambao wamekuwa wakienda katika baadhi ya makampuni kufanya uchunguzi kama kuna watu ambao ni wahamiaji haramu lakini hawafanyi kile ambacho wanatakiwa kukifanya.

“Changamoto kubwa ipo katika Jiji la Dar es Salaam na kwa maana hiyo nimeagiza watu hao waondolewe mara moja na hatua za kinidhamu na kisheria zichukuliwe haraka iwezekanavyo na (kesho) leo zoezi hilo liwe limekamilika” amesema Masauni.

Aidha ameiagiza Idara ya Uhamihaji kuhakikisha inaimarisha ulinzi mipakani ili kutibu tatizo la wahamihaji haramu wanaoingia kutoka nchi za jirani na kukamatiwa katika maeneo ambayo siyo ya mipakani.

Masauni amesema, licha ya kuwa kwa sasa nchi ipo shwari kalini jeshi la polisi linakazi kubwa ya kuhakikisha linaimarisha ulinzi, na kufanya upelelezi wa kina na kwa haraka pale yanapotokea mauaji au uharifu wa aina yoyote.

Kuhusu masuala ya ajira ndani ya wizara hiyo ambazo serikali ilitangaza kuzisitisha, Masauni amesema, kwa sasa baada ya wakuu wa idara zote viongozi waandamizi kukaa, wamekubaliana kurejesha ajira hizo katika Idara ya Uhamiaji na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

“Kwa sasa idara ya uhamiaji ina nafasi za ajira 702 ambazo zinahitaji kujazwa huku Jeshi la Zima moto na uhokoaji zinahitaji ajira 522.

“Kutokana na hali hiyo na kwa kuzingatia kwamba idara hizo zilikuwa hazijakamilisha ajira hizo wakati wa kipindi cha mwaka wa fedha 2015/16 zilikuwa hazijajazwa na hivyo kama ajira zingeendelea kusitishwa vijana wengi wangekosa haki yao nab ado kuna upungufu.

“Vijana wenye sifa sasa wanaweza kuanza kujiandaa kwa ajili ya kufanya maombi pale ambapo nafasi hizo zitaanza kutangazwa katika vyombo vya habari” amesema Masauni.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top