Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SERIKALI KUZITAMBUA NA KUZIRASIMISHA BANDARI BUBU

Serikali imesema kuwa inaendelea na utaratibu wa kuzitambua na kuzirasimisha bandari Bubu zote zilizokidhi vigezo ambazo zinatumiwa na wafanyabiashara kupitisha bidhaa mbalimbali ili ziweze kuchangia katika Pato la Taifa kulingana na  wingi wa bidhaa zinazopitishwa katika bandari hizo.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani ametoa kauli hiyo bungeni mjini Dodoma leo wakati akijibu maswali ya Wabunge waliotaka kujua mkakati wa Serikali katika kudhibiti bidhaa zinazoingizwa nchini na wafanyabiashara wasio waaminifu kupitia bandari bubu hali inayoikosesha  serikali mapato.

Mhe. Ngonyani amekiri kuwepo kwa ongezeko la wafanyabiashara wasio waaminifu wanaotumia bandari hizo katika maeneo mbalimbali nchini hasa ukanda wa Pwani wa Bahari ya Hindi, Ziwa Tanganyika, Ziwa Victoria na maeneo ya mipakani ambayo yanaingia moja kwa moja kwenye makazi ya watu akieleza kuwa wengi wa wafanyabiashara wanakwepa kodi na kutafuta urahisi wa kupitisha mizigo yao.

Amesema maeneo hayo yamekuwa chanzo kikubwa cha upitishaji wa bidhaa zisizokidhi viwango, Silaha na Biashara haramu na kubainisha kuwa baadhi ya wafanyabiashara wa ndani wasio waaminifu wamekuwa wakishirikiana na raia wa kigeni kuagiza na kuingiza bidhaa hizo kupitia bandari hizo kwa lengo la  kukwepa kodi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top