Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SERIKALI YANASA KILO MIL 34 ZA SUKARI MAFICHONI

Shehena ya sukari ya kilo milioni 34 zilizokuwa zimefichwa kwenye maghala ya wafanyabiashara watatu Kilimanjaro imekamatwa na vyombo vya usalama, na serikali mkoani humo imetangaza kuiuza kwa wananchi kuanzia jana kwa bei elekezi ya Sh. 1,800.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Mecki Sadiki alithibitisha jana kukamatwa kwa shehena hiyo, baada ya makachero wanaoongoza timu maalumu ya ukaguzi wa maghala ya wafanyabiashara na mawakala wa sukari kubaini kufichwa kwa bidhaa hiyo.

“Tumefanya ukaguzi katika maghala 45 na katika harakati hizo tumenasa kilo milioni 34 za sukari iliyokuwa imefichwa," alisema.

"Katika zoezi hilo kuna mfanyabiashara mmoja mkubwa, yeye alikutwa na tani 31.33 lakini alikuwa akiiuza, isipokuwa bado tumewapa kazi Mamlaka ya Mapato (TRA) ichunguze kama imehodhiwa isivyo halali,” alisema Sadiki.

Kiasi cha sukari iliyobakia, alisema Mkuu wa M koa huyo, kilikamatwa kwa wafanyabiashara wengine wawili, ambao walikuwa na tani nne kasoro, Moshi mjini na Marangu.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa mkoa, shehena hiyo ya sukari hadi jana mchana ilikuwa ikishikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kiuchunguzi na kwamba ametoa amri igawiwe kwa wananchi kwa bei elekezi iliyotangazwa na serikali.

Kuhusu upungufu wa sukari Kilimanjaro, Sadiki alisema "Sisi kama mkoa tumefanya mawasiliano na mawakala walioko Dar es salaam, ambao sukari yao ilikuwa inashikiliwa na vyombo vya usalama na wametuahidi kuukabili uhaba wa sukari uliopo hapa kwetu.

“Jana (juzi) niliwasiliana na Mmiliki wa Kampuni ya Zakaria Enterprises na amekubali kuwapa bidhaa hiyo mawakala ambao ni wadau wa Kiwanda cha Sukari cha TPC," alisema Sadiki. 

"Kwa hiyo tunakwenda vizuri na tumejipanga kuhakikisha kwamba uhaba huo tunaupatia ufumbuzi wa kudumu.Ila ninawaomba wananchi wangu wawe wavumilivu kwa sasa.

"Mawakala wakubwa wa sukari wa Kilimanjaro na mikoa ya Kanda ya Kaskazini ni mfanyabiashara Vicent Laswai ambaye atapatiwa tani 600 za sukari kutoka Kampuni ya Zakaria,alisema Mkuu wa Mkoa huyo.

Aidha, Laswai atapokea tani 640 toka katika Kampuni ya Mohamed Enterprises, alisema.

Kampuni ya Zakaria pia imekubali kutoa tani 640 kwa Kampuni ya Marenga Investment, alisema Sadiki na kubainisha kuwa Mohamed Enterprises imemuahidi kuziba pengo la upungufu utakaojitokeza.

Tangu Rais Magufuli apige marufuku uingizaji sukari kutoka nje ya nchi Februari 17 mwaka huu, baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu wamekuwa wakificha bidha hiyo kama njia ya kuihadaa serikali kwamba kuna uhaba mkubwa.

Wakati akipiga marufuku, Magufuli alisema kama kutakuwa na uhitaji wa sukari kuingia nchini, vibali atavitoa yeye si mtu mwingine yeyote ili kuviwezesha viwanda vya ndani viendelee kuzalisha bidhaa hiyo, kuendelea kutoa ajira na kuinua kipato cha wakulima wa miwa.

Alisema inasikitisha kuona sukari ikiingizwa nchini kutoka nje wakati nchi ina viwanda vingi vya bidhaa hiyo na kusababisha Watanzania wengi kupoteza ajira kutokana na sukari wanayozalisha kukosa soko.

"Nakuagiza Waziri Mkuu, kuanzia leo, marufuku mtendaji yeyote wa Serikali kutoa kibali cha kuagiza na kuingiza sukari kutoka nje ya nchi...vibali vyote nitatoa mimi," alisema Rais Magufuli.

"Katika kampeni zangu mwaka 2015, nilisema Serikali yangu itakuwa ya viwanda hivyo lazima tuvithamini viwanda vya ndani na kulinda bidhaa zinazozalishwa."
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top