Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SERIKALI YAPOKEA BILIONI 224

Na Tiganya Vincent_MAELEZO-Dodoma.

Jumla ya shilingi bilioni 224.314 (224,314,313,555.30) zimepokelewa na Serikali toka kwa wafadhili ili kusaidia kupunguza athari na kuhimili mabadiliko ya tabianchi.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Naibu Waziri , Ofisi ya Makamu wa Rais ,Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Wawi Mhe. Ahmed Juma Ngwali aliyetaka kujua serikali imeokea kiasi gani toka kwa wafadhili kusaidia kupunguza athari na mabadiliko ya tabianchi tangu 2010 hadi 2015.

Alisema kuwa kati ya fedha hizo shilingi bilioni 7,017(7,017,510,977.40) na shilingi 217.296 (217,296,802,577.90 zilipokelewa moja kwa moja kutoka kwa wadau wengine.Mhe. Mpina alisema kuwa fedha hizo zilipatikana baada ya kuandaa miradi kwa kuzingatia vigezo na viapaumbele vya vyanzo vya fedha husika.

Alisema kuwa kati ya fedha hizo shilingi bilioni 17.2 zilipelekwa Zanzibar kwa ajili miradi ya ujenzi kutwa katika baadhi ya maeneo ya bahari ambayo yameanza kuathirika na upandaji wa mikoko ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.Mhe. Mpina alisema kuwa fedha hizo zimepokelewa kutoka Mifuko iliyo chini ya Mkataba wa Mabadiliko ta Tabianchi na ushirikiano na nchi wafadhili.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top