Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TANI 78 ZA SUKARI ZILIZOSALIMISHWA ZAGAWIWA KWA WANANCHI



Na Woinde Shizza,Arusha 

Jumla ya tani 78 za sukari ambazo zilisalimishwa na baadhi ya wafanya biashara wa kubwa wa sukari katika jiji la Arusha zimegaiwa kwa wananchi wa wilaya ya Arusha mjini ambao walikuwa wanakabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa sukari .

Sukari hiyo ambayo ilisalimishwa na wafanyabiashara wakubwa ambao ni Neema Investment imegaiwa katika jumla ya kata 25 zilizopo katika wilaya ya Arusha mjini huku kila kata ikiwa inapatiwa mifuko 1000 kwa ajili ya wananchi wake .

Akiongea na waandishi wa habari kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Arusha ,Afisa tarafa wa kata ya Suye Felician Mtahengerwa alisema kuwa sukari sukari hiyo inayogaiwa kwa wananchi ni ile ambayo iliingizwa hapa mkoani na baadhi ya wafanya biashara wakubwa na kuisalimisha katika ofisi ya mkuuwa mkoa kama agizo lilivyotolewa .

Alisema kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha alisema kuwa mfanya biashara yeyote wa sukari ambaye anaingiza sukari mkoani hapa anapaswa kutoa taarifa katika ofisi yake kabla ya kufanya kitu chochote ikiwemo kabla ya kuuza sukari hiyo ivyo wafanyabishara hawa waliisalimisha sukari hiyo na ndio ambayo inagaiwa kwa kufuata utaratibu.

Alisema awali walishagawa sukari tani 45 na sasa ivi wanagawa tani zingine 33 ambazo zimetoka kwa mfanyabishara Neema intaprasesi ambayo yeye aliingiza sukari hii mara baada ya serekali kutoa agizo hivyo aliamua kuisalimisha kwa kutoa taarifa katika ofisi ya mkuu wa mkoa na sasa ivi ndio wameigawa .

“kunautaratibu wa wafanyabishara wakubwa wanapoingiza sukar I tu hapa mkoani kutoa taarifa sehemu husika ili sukari ile iweze kugaiwa kwa kufuata utaratibu hivyo huyu alitoa taarifa na ndio maana tumekuja hapa kuungana nae kuakikisha kila kata inapata sukari mifuko 1000 ambayo itauzwa kwa bei halili ya serekali ambayo imeelekezwa”alisema Mtahengerwa.

Alisema kuwa utaratibu huu unaotumika wa kugawa sukari utaendelea hivi hivi na hata sukari ambayo imeagizwa na waziri mkuu iwapo itafika utaratibu huu huu ndio utatumika adi pale tatizo la sukari litakapo malizika kabisa

Alitoa wito kwa wafanyabiashara wakubwa ambao wanaingiza sukari kutoa taarifa katika ofisi husika kwani wakiingiza bila kutoa taarifa iwapo wakibainika watachukuliwa hatua ya kisheria ikiwa ni pamoja na kutaifishiwa sukari yote.

Aidha pia aliwataka wafanya bishara wadogo wadogo ambao wamepata sukari hiyo kuuza kwakufuata bei elekezi kwani wanapokiuka agizo hilo iwapo watabainika wameuza kwa bei ya juu tofauti na bei elekezi sheria kali watachukuliwa ikiwemo ya kuwapeleka mahakamani.

Kwa upande wake mfanyabishara mkuu ambaye alijitambulisha kwa jina la Romanusi Mwacha alisema kuwa yeye kama mfanyabishara mkubwa ameamua kumuunga Rais Magufuli mkono kwa kuanza kuuza sukari kwa bei elekezi japo kuwa amepata hasara kubwa.

Alisema kuwa kama yeye amenunua sukari shilingi 1900 kilo na bado ajaweka bei ya usafiri kutoka aliponunua dar adi hapa lakini kutokana na agizo la serekali ameamua kulifuata na kumuunga magufuli mkono na ndio maana pamoja yakuwa amenunua bei gali lakini anauza bei raisi kwa kilo shilingi 1700 ili mfanyabiashara mdogo anaenunua aweze kwenda kumuuzia mlaji bei ya shilingi 1800 kama serekali ilivyoelekeza.

Aliwasihi wafanyabishara wengine ambao wameficha sukari wazitoe na wale ambao wanauza katika maduka ya reja reja wauze bei elikezi ili kutoweza kumuumiza mlaji ambaye ni mwananchi .
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top