Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

BREAKING NEWS ... RAIS MAGUFULI APANGUA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA ... ATEUA WAKUU WA WILAYA 139 .... BOFYA HAPA KUONA ORODHA KAMILI


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA


KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU




Simu : +255-22-2114512, 2116898


Email : press@ikulu.go.tz


Tovuti : www.ikulu.go.tz


Faksi : 255-22-2113425





OFISI YA RAIS,


IKULU,


1 BARABARA YA BARACK OBAMA,


11400 DAR ES SALAAM,


TANZANIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139
.


Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.


Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.


Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.


Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine.


Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.


Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi wake umetenguliwa.


Wakuu wapya wa mikoa walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya uongozi.


Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 139.


Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika uteuzi huo Rais Magufuli amezingatia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka 60 ameamua wastaafu.


Mhe. Rais amewashukuru sana kwa utumishi wao mzuri na amesema pale ambapo itahitajika, serikali itaendelea kuwatumia katika majukumu mengine.


Katika uteuzi huo, Wakuu wa Wilaya waliopo sasa ambao wamebaki katika nafasi zao ni 39. Pia Rais Magufuli amewateua Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri 22 kuwa Wakuu wa Wilaya kutokana na utendaji wao mzuri.


Aidha, nafasi 78 za uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu katika maeneo mbalimbali.


Walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya ni kama ifuatavyo (Orodha imepangwa kulingana na mikoa)


ARUSHA

Arusha - Mrisho Mashaka Gambo

Arumeru - Alexander Pastory Mnyeti

Ngorongoro - Rashid Mfaume Taka

Longido - Daniel Geofrey Chongolo

Monduli - Idd Hassan Kimanta

Karatu - Therezia Jonathan Mahongo






DAR ES SALAAM

Kinondoni - Ally Hapi

Ilala - Sophia Mjema

Temeke - Felix Jackson Lyaviva

Kigamboni - Hashim Shaibu Mgandilwa

Ubungo - Hamphrey Polepole




DODOMA

Chamwino - Vumilia Justine Nyamoga

Dodoma - Christina Solomon Mndeme

Chemba - Simon Ezekiel Odunga

Kondoa - Sezeria Veneranda Makutta

Bahi - Elizabeth Simon

Mpwapwa - Jabir Mussa Shekimweli

Kongwa - John Ernest Palingo




GEITA

Bukombe - Josephat Maganga

Mbogwe - Matha John Mkupasi

Nyang'wale - Hamim Buzohera Gwiyama

Geita - Herman C. Kipufi

Chato - Shaaban Athuman Ntarambe




IRINGA

Mufindi - Jamhuri David William

Kilolo - Asia Juma Abdallah

Iringa - Richard Kasesela




KAGERA

Biharamulo - Saada Abraham Mallunde

Karagwe - Geofrey Muheluka Ayoub

Muleba - Richard Henry Ruyango

Kyerwa - Col. Shaban Ilangu Lissu

Bukoba - Deodatus Lucas Kinawilo

Ngara - Lt. Col. Michael M. Mtenjele

Missenyi - Lt. Col Denis F. Mwila




KATAVI

Mlele - Rachiel Stephano Kasanda

Mpanda - Lilian Charles Matinga

Tanganyika - Saleh Mbwana Mhando




KIGOMA

Kigoma - Samsoni Renard Anga

Kasulu - Col. Martin Elia Mkisi

Kakonko - Col. Hosea Malonda Ndagala

Uvinza - Mwanamvua Hoza Mlindoko

Buhigwe - Col. Elisha Marco Gagisti

Kibondo - Luis Peter Bura




KILIMANJARO

Siha - Onesmo Buswelu

Moshi - Kippi Warioba

Mwanga - Aaron Yeseya Mmbago

Rombo - Fatma Hassan Toufiq

Hai - Gelasius Byakanwa

Same - Rosemary Senyamule Sitaki




LINDI

Nachingwea - Rukia Akhibu Muwango

Ruangwa - Joseph Joseph Mkirikiti

Liwale - Sarah Vicent Chiwamba

Lindi - Shaibu Issa Ndemanga

Kilwa - Christopher Emil Ngubiagai






MANYARA

Babati - Raymond H. Mushi

Mbulu - Chelestion Simba M. Mofungu

Hanang' - Sara Msafiri Ally

Kiteto - Tumaini Benson Magessa

Simanjiro - Zephania Adriano Chaula




MARA

Rorya - Simon K. Chacha

Serengeti - Emile Yotham Ntakamulenga

Bunda - Lydia Simeon Bupilipili

Butiama - Anarose Nyamubi

Tarime - Glodious Benard Luoga

Musoma - Dkt. Vicent Anney Naano




MBEYA

Chunya - Rehema Manase Madusa

Kyela - Claudia Undalusyege Kitta

Mbeya - William Ntinika Paul

Rungwe - Chalya Julius Nyangidu

Mbarali - Reuben Ndiza Mfune




MOROGORO

Gairo - Siriel Shaid Mchembe

Kilombero - James Mugendi Ihunyo

Mvomero - Mohamed Mussa Utali

Morogoro - Regina Reginald Chonjo

Ulanga - Kassema Jacob Joseph

Kilosa - Adam Idd Mgoyi

Malinyi - Majula Mateko Kasika




MTWARA

Newala - Aziza Ally Mangosongo

Nanyumbu - Joakim Wangabo

Mtwara - Dkt. Khatibu Malimi Kazungu

Masasi - Seleman Mzee Seleman

Tandahimba - Sebastian M. Walyuba




MWANZA

Ilemela - Dkt. Leonald Moses Massale

Kwimba - Mhandisi Mtemi Msafiri Simeon

Sengerema - Emmanuel Enock Kipole

Nyamagana - Mary Tesha Onesmo

Magu - Hadija Rashid Nyembo

Ukerewe - Estomihn Fransis Chang'ah

Misungwi - Juma Sweda




NJOMBE

Njombe - Ruth Blasio Msafiri

Ludewa - Andrea Axwesso Tsere

Wanging'ombe - Ally Mohamed Kassige

Makete - Veronica Kessy




PWANI

Bagamoyo - Alhaji Majid Hemed Mwanga

Mkuranga - Filberto H. Sanga

Rufiji - Juma Abdallah Njwayo

Mafia - Shaibu Ahamed Nunduma

Kibaha - Asumpter Nsunju Mshama

Kisarawe - Happyness Seneda William

Kibiti - Gulamu Hussein Shaban Kifu




RUKWA

Sumbawanga - Dkt. Khalfan Boniface Haule

Nkasi - Said Mohamed Mtanda

Kalambo - Julieth Nkembanyi Binyura




RUVUMA

Namtumbo - Luckness Adrian Amlima

Mbinga - Cosmas Nyano Nshenye

Nyasa - Isabera Octava Chilumba

Tunduru - Juma Homela

Songea - Polet Kamando Mgema




SHINYANGA

Kishapu - Nyambonga Daudi Taraba

Kahama - Fadhili Nkulu

Shinyanga - Josephine Rabby Matiro






SIMIYU

Busega - Tano Seif Mwera

Maswa - Sefu Abdallah Shekalaghe

Bariadi - Festo Sheimu Kiswaga

Meatu - Joseph Elieza Chilongani

Itilima - Benson Salehe Kilangi






SINGIDA

Mkalama - Jackson Jonas Masako

Manyoni - Mwembe Idephonce Geofrey

Singida - Elias Choro John Tarimo

Ikungi - Fikiri Avias Said

Iramba - Emmanuel Jumanne Luhahula




SONGWE

Songwe - Samwel Jeremiah

Ileje - Joseph Modest Mkude

Mbozi - Ally Masoud Maswanya

Momba - Juma Said Irando






TABORA

Nzega - Geofrey William Ngudula

Kaliua - Busalama Abel Yeji

Igunga - Mwaipopo John Gabriel

Sikonge - Peres Boniphace Magiri

Tabora - Queen Mwashinga Mlozi

Urambo - Angelina John Kwingwa

Uyui - Gabriel Simon Mnyele




TANGA

Tanga - Thobias Mwilapwa

Muheza - Mhandisi Mwanaisha Rajab Tumbo

Mkinga - Yona Lucas Maki

Pangani - Zainab Abdallah Issa

Handeni - Godwin Crydon Gondwe

Korogwe - Robert Gabriel

Kilindi - Sauda Salum Mtondoo

Lushoto - Januari Sigareti Lugangika


Wakuu wote wa Wilaya walioteuliwa wanapaswa kufika Ikulu Dar es salaam siku ya Jumatano tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi kwa ajili ya kiapo cha maadili ya uongozi na maelekezo mengine kabla ya kuapishwa na wakuu wa mikoa watakaporejea katika mikoa yao.


Gerson Msigwa


Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU


Dar es salaam


26 Juni, 2016
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top