Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SAKATA LA MAUAJI YA DADA YAKE BILIONEA MSUYA LACHUKUA SURA MPYA

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam limetuma timu ya maofisa wake kwenda mikoa ya Arusha na Mwanza kufanya upelelezi wa mauaji ya dada wa bilionea Erasto Msuya, Aneth Msuya. 

Hadi sasa jeshi hilo limewakamata watu wanne kwa tuhuma za mauaji hayo, akiwamo mumewe Aneth, mfanyakazi wao wa ndani na hawara wa mfanyakazi huyo.

Kamanda Sirro hakumtaja mtuhumiwa wa nne aliyekamatwa kwa tuhuma za mauaji hayo yaliyogusa hisia za watu. 

Aneth aliuawa kwa kuchinjwa na watu wasiojuliana Mei 26 mwaka huu, nyumbani kwake Kibada Kigamboni jijini Dar es Salaam, ambao inadaiwa hawakuchukua kitu chochote ndani na kutoweka. 

Sirro alisema alituma maofisa hao kwenda Mwanza na Arusha kufanya upelelezi wa mauaji ya Aneth ili kubaini chanzo chake.

Hata hivyo, hakutaka kufafanua zaidi sababu za kutuma timu hiyo kwenye mikoa hiyo wakati mauaji hayo yalifanyika jijini Dar es Salaam. 

“Jeshi la polisi bado tunafuatilia, kwa sasa tumeshatuma maofisa wetu wameenda katika mkoa wa Mwanza na Arusha ili kufanya upelelezi zaidi,”alisema Sirro. 

Alisema jeshi hilo linaendelea kuwahoji watuhumiwa wanaowashikilia ili kubaini chanzo cha mauaji hayo, hivyo upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani.

Bilionea Msuya aliuawa kwa kupigwa risasi zaidi ya 12 na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi kandokando ya barabara eneo la Mojohoroni wilayani Hai Mkoa wa Kilimanjaro.

Februari 10, mawakili wanaosimamia kesi ya bilionea huyo, Hudson Ndusyepo, Majura Magafu, Emmanuel Safari na John Lundu, waliiambia mahakama kuwa Serikali inakusudia kuita mashahidi 50 kuthibitisha mashtaka na kuwasilisha vielelezo 40, ikiwamo bunduki iliyotumika katika mauaji hayo.

Mawakili hao walidai mipango ya kumuua bilionea Msuya ilianza Julai 26, mwaka 2013 jijini Arusha, ikiwahusisha washtakiwa hao baada ya kuahidiwa wangelipwa Sh5 milioni kila mmoja.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top