Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SUMU YASABABISHA KIKAO CHA MEYA WA JIJI MWANZA KUVUNJIKA

Kikao cha kamati ya fedha na uongozi cha halmashauri ya jiji la Mwanza, kimevunjika baada ya Meya wa jiji hilo James Bwire kulalamikia harufu kali, inayohisiwa kuwa ni sumu iliyokuwa ikitoka kwenye kiyoyozi ndani ya ofisi yake, huku watumishi wawili wa jiji hilo wakishikiliwa na polisi kwa mahojiano zaidi.

Mkurugenzi wa jiji la Mwanza, Adam Mgoyi amethibitisha kusambaratika kwa wajumbe wa kikao hicho.

Watumishi wanaohojiwa na jeshi la polisi ni katibu muhtasi wa ofisi ya mstahiki Meya Gladys Chiduo pamoja na karani wa ofisi hiyo Anselemi Mtobesya.

Mstahiki Meya James Bwire, ambaye mwezi aprili mwaka huu alilazwa katika hospitali moja jijini Nairobi nchini Kenya kwa muda wa mwezi mmoja baada ya kudaiwa kuanguka ghafla ofisini kwake, anaeleza hali aliyoikuta ofisini kwake wakati alipoingia maliwatoni kwa ajili ya kujisaidia wakati kikao hicho kilipokuwa kinaendelea.

Diwani wa kata ya Mbugani Mahamoud Jama pamoja na Hanifa Mhere ambaye ni diwani wa viti maalum wanasimulia kwa kina kuhusiana na tukio hilo ambalo limetokea hii leo baada ya wajumbe wa kamati hiyo kumaliza kutembelea miradi ya jiji iliyopo eneo la Community Centre kata ya Mirongo na Sinai kata ya Mabatini ambako eneo kwa ajili ya machinga limetengwa.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top