Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAZIRI WA KILIMO CHARLES TIZEBA ATUMBUA WAKURUGENZI WATANO

WAZIRI wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles Tizeba amewasimamisha kazi wakurugenzi watano wa idara tofauti katika wizara hiyo kutokana na kuonesha udhaifu mbalimbali katika utendaji wao na wengine kusababisha hasara katika usalama wa chakula.

Waliosimamishwa kazi ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Chakula nchini, Ombaeli Lemweli kutokana na kutoa vibali vya ununuzi wa mazao na kuuzwa nje ya nchi ilhali tathmini ikiwa haijafanyika. Nafasi yake kuchukuliwa na Elimpaa Kiranga aliyekuwa Mkurugenzi wa Bodi ya Mazao Mchanganyiko.

Aidha, ameagiza kusimamishwa kazi kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), Charles Walwa na nafasi yake kushikwa na Deusdedit Mpazi aliyekuwa Meneja wa NFRA kanda ya Dodoma, kutokana na kuharibu ghala la chakula na kusababisha hasara.

Viongozi wengine wa NFRA waliosimamishwa ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Huduma, Anna Ngoo, Mkurugenzi wa Masoko, Mikalu Mapunda na Meneja wa NFRA, Songea Jeremia Mtafya ambao wametakiwa kupisha na uchunguzi kufanyika mara moja dhidi yao.

Kadhalika, Dk Tizeba amemsimamisha kazi aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bahari Kuu, Rashid Hoza na nafasi yake kushikwa na Hosea Mbilinyi aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi, lengo likiwa ni kuimarisha ulinzi wa Bahari Kuu.

Mbali na nafasi hizo, pia Mkuu wa Kituo cha Utafiti cha Uyole mkoani Mbeya, Dk Zakaria Maly amevuliwa madaraka na kuhamishiwa katika Kituo cha Utafiti Seliani mkoani Arusha kuendelea na utafiti na badala yake nafasi yake itachukuliwa na Arnold Msongi anayetoka Kituo cha Utafiti Ilonga, Kilosa mkoani Morogoro.

Dk Tizeba alitoa maamuzi hayo jana Dar es Salaam wakati akizungumzia masuala mbalimbali, ikiwa ni mwezi mmoja baada yakuteuliwa na Rais John Magufuli kushika wadhifa huo katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri yaliyompeleka aliyekuwa waziri wa wizara hiyo, Mwigulu Nchemba kuongoza Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Waziri Tizeba alisema wakati ambapo tathmini ya chakula nchini ikiwa haijakamilika, Kurugenzi ya Usalama wa Chakula imekuwa ikitoa vibali vya chakula kusafirishwa nje ya nchi, huku ikiwa haijulikani kama chakula kilicho kinatosha au hakitoshi na ili ziada ilindwe.

“Mbali ya kwamba hali ya chakula nchini ni nzuri lakini kumekuwepo na wimbi la wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi wakipewa vibali na kununua mazao ndani ya nchi na kuyauza nje ilhali tathmini ikiwa haijakamilika,” alisema Tizeba.

Alitoa wiki mbili kuanzia sasa ukaguzi wa chakula nchini uwe umefanyika ili kupatikana kwa tathmini halisi katika kipindi cha mwaka 2015/2016 kwani ununuzi wa mazao hayo umeonekana mkubwa na hali hiyo isipodhibitiwa hali itakuwa mbaya zaidi.

Alisema vibali hivyo vimekuwa vikitolewa kinyume cha utaratibu kwa kuwa tathimini ilitakiwa kufanyika kwanza, hivyo Katibu Mkuu amsimamishe kazi mkurugenzi huyo na uchunguzi ufanyike dhidi yake pamoja na vibali ambavyo vimekuwa vikitolewa tangu mwaka jana kwani havina harufu nzuri.

“Hata hivi karibuni nimepata taarifa kuna mfanyabiashara kapewa kibali cha kusafirisha tani laki tatu kupeleka nchini Malawi, mfanye uchunguzi wa vibali vyote alivyovitoa,” alisema Tizeba.

Kuhusu NFRA, Dk Tizeba alisema umekuwepo udhaifu mkubwa katika ghala la Songea, Dodoma na Sumbawanga ambako mazao yameharibika na kusababisha hasara huku uongozi wa wakala licha ya kuombwa vibali vya kununuliwa kwa mazao hayo kama chakula cha mifugo havikutolewa.

Akizungumzia uvuvi bahari kuu, ameiagiza Kurugenzi wa Uvuvi kubadilisha masharti ya leseni ya uvuvi katika bahari kuu ili kuangalia uwezekano wa kufanya ubia na wavuvi hao ili Watanzania nao waweze kunufaika na mavuno ya mazao hayo.

Alisema kwa wale ambao wana leseni hazitofanyiwa mabadiliko lakini kwa zile mpya na sheria haizuii kufanya hivyo.

Alisema hivi sasa zipo meli 105 zote zikitoka nje ya nchi zikiwa zinaendelea na uvuvi na kuchota chochote na kuondoka, huku mamlaka ya bahari wakiwa wanayajua hayo, wakidai kuwa Tanzania haina mahali pa kushushia.

Alisema kuanzia sasa meli zote ziambiwe mazao yote watakayovuna ambayo ni tofauti na leseni zao zinavyotaka yaletwe Dar es Salaam, yagawiwe kama itakavyohitajika kwani Tanzania imeendelea kuwa shamba la bibi kutokana na kukosa uwezo wa kuvua katika bahari kuu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top