Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

HALI TETE .... TAARIFA KAMILI JUU YA MAAZIMIO YA MKUTANO WA DHARURA WA YANGA

Viongozi wa klabu ya Yanga leo saa nne walikutana katika kikao cha dharura kufuatia mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji kutangaza kujiuzulu na kutupilia mbali mpango wake wa kutaka kuikodisha timu hiyo na kuiendesha kibiashara kwa miaka 10.

Manji alijiuzulu kwa tuhuma kuwa kuna baaadhi ya viongozi wa Yanga wamemkashafu na mmoja aliyetuhumiwa kwa kosa hilo ni Katibu Mkuu wa Baraza la Wazee, Yahya Akilimali.

Maazimio ya Viongozi wa Matawi wa Yanga waliokutana leo katika kikao cha dharura Makao Makuu ya Yanga.

1. Viongozi hao wamelaani taarifa iliyotolewa katika vyombo vya habari na Katibu wa Baraza la Wazee, Mzee Akilimali na kuwa haikuwa taarifa iliyopewa baraka na Yanga.

2. Viongozi wa Matawi wamemtaka Katibu Mkuu wa Yanga kumfuta uanachama wa Yanga Yahya Akilimali kwa kosa la kumkashifu mwenyekiti wa Yanga.

3. Katiba ya Yanga hailitambui Baraza la Wazee badala yake inalitambua Baraza la Wadhamini, hivyo basi viongozi wa Yanga wamemuomba Katibu Mkuu wa Yanga kuvunja Baraza la Wazee na wazee hao warudishwe katika matawi wawe wanachama wa kawaida.

4. Mwanachama yeyote wa Yanga atakayeongea na vyombo vya habari bila idhini ya Yanga, atakuwa amejifuta uanachama wake.

Kwa upande wa Mzee Yahya Akilimali alikuwa na haya ya kusema;-

Sijamtusi mwenyekiti wangu kwa kusema amekurupuka. Neno hilo ni la kawaida wala sikuwa na dhamira ya kumtusi mwenyekiti wangu, nawaomba radhi wana-Yanga kwa kauli zangu. Usiku sijalala nilikosa raha mara baada ya kusikia Manji kajiuzulu. 

Mie naomba tuwe na umoja tatizo letu na mwenyekiti ni kushindwa kutuita wazee kwenye mpango wake wa kuichukua timu. 

Sisi tunampenda na kumuhitaji sana Yusuf lakini tunahitaji aendeleze mfumo wa zamani alioanza nao wa kujali na kuthamini wazee ili nasi tujisikie vizuri na klabu yetu. 

Nasisitiza sina chuki na Manji maana kwa mdomo wangu huu nimeshiriki sana kumuweka madarakani mpaka pale umma wa watanzania wakasema tumevunja katiba. Ninachotaka alitambue Baraza la Wazee na sisi tukae nae tuzungumze mstakabali wa klabu yetu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top