Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAZIRI NCHEMBA AAPA KUPAMBANA NA WAUZA MADAWA YA KULEVYA

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba ametoa siku 14 kwa maofisa wanaohusika na udhibiti wa dawa za kulevya kwenye mpaka wa Tunduma mkoa wa Songwe, kuwakamata watu wanaohusika na uvushaji wa dawa hizo kutoka nchini kwenda nchi jirani ya Zambia na nyingine zilizopo ukanda huo.

Nchemba alitoa agizo hilo jana, alipofanya ziara ya kukagua mpaka huo, ambapo alisema ni jambo lisilofichika kuwa kwa sasa Tanzania imechafuka kutokana na dawa za kulevya.

Alisema kutokana na Watanzania wengi kukamatwa katika nchi mbalimbali duniani, wakijihusisha na usafirishaji wa dawa za kulevya, imefikia hatua kwa baadhi ya nchi kufikiria kuongeza masharti zaidi kwa kila atakayejitambulisha kuwa Mtanzania.

“Hatuwezi kuacha nchi ikachafuka kwa sababu tu ya watu wachache.Ukienda China Watanzania zaidi ya 200 wanashikiliwa kwa dawa za kulevya, Pakistan wapo, India, Afrika Kusini ni Watanzania. Hili linatuchafua sana,”alisema Nchemba.

Aliutaja mpaka wa Tunduma kuwa miongoni mwa maeneo yanayoongoza kwa kupitisha dawa hizo na kutaka nguvu kuongezwa zaidi ili kuwezesha misako.

Alisema wapo watu ambao si makondakta wa mabasi wala abiria, lakini wamekuwa wakisafiri kila siku kwenye mabasi, hatua inayodhihirisha kuwa ndiyo wanaojihusisha na usafirishaji wa bidhaa hizo haramu.

Alisema watu hao wamekuwa na ushirikiano na watu wengine katika miji ya jirani, kabla ya kufika mpakani ikiwemo kijiji cha Mpemba wilayani Momba mkoani Songwe, ambapo wakifika hapo basi husimamishwa na mzigo kushushwa, kisha kusafirishwa kwa njia za panya hadi ng’ambo ya nchi.

“Wakati ninyi mnafanya utaratibu wa kawaida wa kupitisha gari husika hapa mpakani, wao wanavusha kupitia njia za panya. Basi likishavuka na mzigo unakuwa umefika Zambia wanakutana na kuupakia tena kisha wanaendelea na safari. 

“Na katika hili ni lazima mzungumze pia na wenzenu wa upande wa pili, wadhibiti pia mji unaofuata baada ya huo wa mpakani maana huko ndiko wanakopakia tena. Kama mtashindwa katika wiki mbili, nitakuja mimi mwenyewe na nitawakamata tu,” alisisitiza.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top