Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Cheche alizozitema Rais Magufuli wakati anazindua ndege 2 mpya



=> Rais Magufuli: Lakini unaweza ukajiuliza, ndege hii imetoka Canada imefika hapa, watu wanasema hazina spidi, ni bajaji.

 => Rais Magufuli: Ndege hizi hazitumiki tu Tanzania, Marekani wana ndege zaidi ya 40 za aina hii, Misri wanazo-

 => Rais Magufuli: Ukitaka kujenga uchumi, kuinua utalii, huwezi kufanya kama taifa halina ndege- Rais

 => Rais Magufuli: Ndege ya Jeti, kutoka Dar hadi Mbeya mafuta ni milioni 28, lakini hizi ni milioni moja

 => Rais Magufuli: Kama mtu anaona ana haraka sana ya kuwahi anapokwenda, akapande ndege za jeshi awahi

 => Rais Magufuli: Kutoka Dar hadi Mbeya, tofauti ya muda wa kufika kati ya ndege hii na Jet ni dakika 20 tu-

 => Rais Magufuli: Niwaombe watanzania tusipende kubeza, kama kitu hukitaki, basi ukae kimya

 => Rais Magufuli: Tungenunua ndege hizi kwa kulipa polepole, tungekuja kulipa gharama kubwa, ndio maana tumelipa zote

 => Rais Magufuli: Tuna mpango wa kununua ndege mbili kubwa, moja itabeba watu 160, nyingine itabeba watu 240

 => Rais Magufuli: Tuliamua kununua ndege, tutazikodisha kwa ATCL, mwendo wa kucheza sasa umekwisha

 => Rais Magufuli: ATCL ilikuwa haijiendeshi kibishara, walikuwa wapo tu, wanategemea serikali kila kitu

 => Rais Magufuli: ATCL haikuwa ikijenga uchumi wa nchi na utalii kama ilivyokuwa inatakiwa

 => Rais Magufuli: Maofisa wa ATCL walikuwa wakijilipa posho za TZS 50,000 kila wakitembelea uwanja wa ndege Dar-

 => Rais Magufuli: Vituo vya ATCL vya Comoro, Mwanza, Mtwara na Dar es Salaam, vilikithiri kwa ubadhirifu

 => Rais Magufuli: ATCL walikuwa hawafuati ratiba, unaweza kuambiwa ndege inaondoka leo, lakini isiondoke hadi wiki moja

 => Rais Magufuli: ATCL walikuwa wakijilipa overtime za uongo

 => Rais Magufuli: ATCL walikuwa wakinunua mafuta hewa, unaambiwa ndege imeenda Mwanza kumbe iko Dar es Salaam uwanjani

 => Rais Magufuli: Katika kituo cha Comoro, ilipotea TZS milioni 700, aliyepoteza akaongezewa muda ili apoteze nyingine

 => Rais Magufuli: Bodi ya ATCL naomba mchambuwe wafanyakazi, chambueni kama Saida Karoli anavyosema, chambua kama karanga

 => Rais Magufuli: Bodi ya ATCL msiogope kupunguza wafanyakazi, tulipunguza 500 wa NIDA, hawa hawatatushinda

 => Rais Magufuli: Mfanyakazi kama unataka kuendelea kufanya kazi ATCL, utubu, uwe tayari kuwatumikia watanzania

 => Rais Magufuli: Ndani ya ATCL kuna wake wa Mawaziri, Shirika halizalishi lakini wake wa Mawaziri wameng'ang'ani tu

 => Rais Magufuli: Wale ambao hawawezi kwenda na mwendo wetu, waje tuwalipe fedha zao watuache tufanyekazi

 => Rais Magufuli: Haiwezekani wageni wakitaka kuja Tanzania, lazima watue nchi nyingine, hii ni aibu kubwa

 => Rais Magufuli: Lakini mjue mnaenda kwenye ushindani, washindani wenu hawatawafurahia, mjipange vizuri kuwakabili-

 => Rais Magufuli: Niwaombe Bodi ya ATCL, msitumie mawakala kukatisha tiketi zenu

 => Rais Magufuli: Kuna wafanyakazi wa ATCL naona wapo wanafanya kazi tangu mimi nipo shule ya msingi

 => Rais Magufuli: ATCL ya sasa ukiona hata sare za wafanyakazi zinatia kichefuchefu, hazitamaniki

 => Rais Magufuli: Lakini niwaombe Watanzania tuwe wazalendo, tutumie usafiri wa ATCL ili tuweze kununua ndege nyingine

 => Rais Magufuli: Niwaombe Bodi na Menejimenti, msimruhusu kiongozi asafiri bure, hata kama ni mimi, mnitoze nauli

 => Rais Magufuli: Najua kunawakati ATCL mnajipendekeza kwa viongozi, lakini mjue mwishoni tutawapima kwa utendaji wenu

 => Rais Magufuli: Hata kama ni kiongozi wa ATCL, ukisafiri hakikisha unalipa nauli, vitu vya bure ndivyo vinatumaliza-

 => Rais Magufuli: Sasa tuna kazi ya kukarabati viwanja, shughuli hii tutaianza mapema sababu fedha tunazo

 => Rais Magufuli: Sisi hatutaki kufukuza wafanyakazi, lakini watajifukuzisha wenyewe kutokana na utendaji wao

 => Rais Magufuli: Ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Dar- Mwanza- Kigali- Bujumbura tayari tenda zimetangazwa

 => Rais Magufuli: Tunataka kuanza ujenzi wa treni za umeme Dar es Salaam, haya si Ulaya tu, hata hapa yatafanyika

 => Rais Magufuli: Ujenzi wa daraja la Coco Beach hadi Agha Khan umeanza, Interchange ya Ubungo itaanza karibuni

 => Rais Magufuli: Mkoa wa Dar es Salaam, una jumla ya wanafunzi hewa 7000, Wafanyakazi hewa wapo 17,000

 => Rais Magufuli: Hii nchi ilikuwa imefika pabaya, kila kona ukigeuka ni hewa, hewa, hewa

 => Rais Magufuli: RAS, DED tuliowafukuza jana, leo wamefikishwa mahakamani, hii imesaidia Uingereza kutuchangia bilioni 6

 => Rais Magufuli: Uingereza imetuchangia bilioni 6 sababu wameona wakitupa fedha zao zitafika kwa walengwa kule Kagera

 => Rais Magufuli: Tunakagua vyeti ili kujua viwango vya elimu na sehemu watu waliposoma, lengo si kuwafukuza wafanyakazi

 => Rais Magufuli: Ndugu zangu kazi hii ni ngumu, Mawaziri msiwaone, hawana raha hawa

 => Rais Magufuli: Waandishi wa habari, ninyi ni muhimili kama ilivyo Bunge, tusaidiane tunapochukua hatua-

 => Rais Magufuli: Waandishi wakati mwingine mnaandika habari za uongo kama nyie mna mahali pengine pakuishi ila si hapa

 => Rais Magufuli: Watanzania mjue, tukishindwa sisi, tumeshindwa sote, tukiweza tumeweza wote

 => Rais Magufuli: No research, no right to speak, lakini hapa ni kinyume, watu hawajui lakini wanaongoza kuongea

 => Rais Magufuli: Kama kungewezekana mtu ukiwa Rais baada ya miaka miwili na nusu unamuachia mwingine, mimi ningefurahi-

 => Rais Magufuli: Natamani huyo aliyesema hazina spidi nimjue nimlipie nauli akae mbele aone zinavyokata mawingu-

 => Rais Magufuli: Ninaishukuru CCM kwa kuandika ilani inayotekelezeka, naamini tutafanya zaidi

 => Rais Magufuli: Mungu ibariki ATCL, Mungu bariki Bodi ya ATCL, Mungu bariki wafanyakazi wazuri, Mungu ibariki Tanzania


Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top