Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ZITTO KABWE AIPONGEZA SERIKALI UNUNUZI WA NDEGE NA MABEHEWA.



Pamoja na kukupa muda ufanye maamuzi kuhusu mambo haya ya TEGETA Escrow, ndg. Rais tunakupongeza sana Kwa kutimiza ahadi yako ya kuleta ndege Kwa ajili ya ATCL. Licha ya kwamba wengine tuna mashaka na bei za ndege hizo, lakini angalau kuna hatua tumepiga. Sisi tunaotoka Kigoma Kwa kweli gharama zitapungua kwani uchache wa ndege unasababisha bei kuwa kubwa sana.

Pia tunakupongeza Kwa kuwezesha kununua mabehewa mapya ya Gari Moshi kwenda Kigoma/Mwanza. Hizi sio hatua za kubeza kwani zitasaidia sana Wananchi kwenye usafiri. Ndugu Rais tunashukuru sana na ninakupongeza Kwa juhudi hizi mahususi.

Hata hivyo tutaendelea kufuatilia Kwa kuchunguza manunuzi haya kwani ndio Kazi yetu Sisi wengine ' kuisimamia Serikali '. Tukikukosoa usikasirike kwani hakuna uzalendo uliyo bora zaidi ya kuikosoa Serikali.

Kudos Kwa ndege na mabehewa. Kazi iendelee
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top