Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CCM wamdhibiti Maalim Seif

Serikali  ya Mapinduzi Zanzibar, imepiga marufuku wanasiasa kutumia nyumba za ibada kwa shughuli za kisiasa Visiwani Zanzibar.

Msimamo huo wa Serikali umekuja siku chache tangu Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, kutumia kila siku za Ijumaa kufikisha ujumbe katika msikiti atakaoswali.

Akitoa tamko la Serikali jana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohammed Aboud Mohammed alisema Serikali inawaagiza wakuu wa mikoa yote ya Zanzibar kusimamia utekelezaji wa agizo hilo katika mikoa yao.

“Kwa taarifa hii Serikali inawaagiza wakuu wa mikoa kupitia kamati zao za ulinzi na usalama kusimamia utekelezaji wa agizo hili katika mikoa yao,” alisema Waziri Aboud.

Alisema Serikali imewaagiza wakuu hao wa mikoa kuchukua hatua za kisheria kwa mtu yeyote atakayekiuka agizo hilo.

Waziri Aboud alisema kwamba viongozi wa dini na kamati zao katika nyumba za ibada watakaoruhusu  wanasiasa kuendesha shughuli za kisiasa watawajibika kwa mujibu wa sheria za nchi.

Alisema kwamba hivi karibuni katika baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja katika Misikiti ya Mbuyuni, Kihibnani na Kwabiziredi kumetokea tabia  kwa baadhi ya viongozi wa kisiasa kupita na kutoa hotuba za kisiasa katika misikiti hiyo.

Waziri huyo alisema kwamba shughuli za vyama vya siasa zinaendeshwa chini ya sheria N0 5 ya mwaka 1992 ambayo imeeleza wazi mipaka na shughuli za kisiasa ziendeshwe chini ya sheria hiyo.

“Vitendo vinavyofanywa na viongozi hao  wa kisiasa wanaotumia nyumba za ibada kama majukwaa ya kisiasa  wanakwenda kinyume na dhamira ya katiba na sheria za nchi ikiwemo sheria ya vyama vya siasa namba 5 ya mwaka 1992” Alisisitiza Waziri Aboud.

Waziri Aboud alisema kwamba shughuli zote za  dini ya kiislamu Zanzibar zinasimamiwa kupitia sheria namba 9 ya mwaka 2001, namba 2 ya mwaka 2007 na namba 3 ya mwaka 1985 zinazoongoza Taasisi mahsusi kama vile Ofisi ya Mufti, Ofisi ya Mahakama ya Kadhi na Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana.

Alisema  kupitia katiba na sheria , uhuru wa mtu kuabudu dini anayoitaka umetolewa bila kuingiliwa na itikadi za vyama vya siasa kama inavyobainishwa  na katiba zote mbili ibara ya 19 ambazo zinaeleza umuhimu wa uhuru wa mtu kuamini dini aitakayo kwa misingi ya kukuza usalama na amani katika jamii.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top